Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
KOCHA Mkuu wa Simba SC, Mzambia, Patrick Phiri amesema kwamba anaijua vizuri Yanga SC na kuelekea mpambano baina yao Oktoba 18, hana wasiwasi hata chembe.
Phiri amesema kwamba aliuangalia vizuri mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC ikifungwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar mjini Morogoro na akaangalia mchezo mwingine, wakiifunga Azam FC 3-0.
“Kwa mechi hizi mbili imetosha kuijua Yanga SC, inatosha kwangu kwa kujipanga kwa ajili ya mechi na wao na sina wasiwasi hata kidogo,”amesema Phiri akihojiwa na BIN ZUBEIRY jana.
KOCHA Mkuu wa Simba SC, Mzambia, Patrick Phiri amesema kwamba anaijua vizuri Yanga SC na kuelekea mpambano baina yao Oktoba 18, hana wasiwasi hata chembe.
Phiri amesema kwamba aliuangalia vizuri mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC ikifungwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar mjini Morogoro na akaangalia mchezo mwingine, wakiifunga Azam FC 3-0.
“Kwa mechi hizi mbili imetosha kuijua Yanga SC, inatosha kwangu kwa kujipanga kwa ajili ya mechi na wao na sina wasiwasi hata kidogo,”amesema Phiri akihojiwa na BIN ZUBEIRY jana.
Hata hivyo, Mzambia huyo amesema kwamba kwa sasa kitu muhimu zaidi ni kutatua matatizo yaliyopo ndani ya Simba SC na si kuanza kuifikiria Yanga SC.
“Tuna matatizo ndani ya Simba SC, hicho ndiyo kitu cha kwanza nitaanza kufanyia kazi katika maandalizi yetu, baada ya hapo ndipo tutawaangalia Yanga wanachezaje,”amesema.
Simba SC inaanza mazoezi leo baada ya mapumziko ya siku mbili tangu icheze na Stand United Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kutoa sare ya 1-1.
Hiyo ilikuwa ni sare ya tatu mfululizo kikosi cha Kocha Patrick Phiri katika mechi zote tatu za mwanzo za Ligi Kuu, baada ya awali kutoka 2-2 na Coastal Union na 1-1 pia na Polisi Moro.
Sare huzo mfululizo hakika zimewashitua viongozi, benchi la ufundi, wachezaji na hata wapenzi na mashabiki wa Simba, hususan timu ikielekea katika mchezo na mahasimu, Yanga SC Oktoba 18.
Phiri aliyerejea Simba SC Agosti mwaka huu kurithi mikoba ya Mcroatia, Zdravko Logarusic aliyefukuzwa- hadi sasa amekwishaiongoza timu hiyo katika mechi tisa, kati ya hizo akishinda nne kufungwa moja na sare nne.
Jana, kocha wa Yanga SC, Mbrazil Marcio Maximo alikaririwa na BIN ZUBEIRY akisema kwamba hawahofii Simba SC kuelekea mchezo huo- ingawa anawahehimu kama timu nzuri na kongwe.
“Tuna matatizo ndani ya Simba SC, hicho ndiyo kitu cha kwanza nitaanza kufanyia kazi katika maandalizi yetu, baada ya hapo ndipo tutawaangalia Yanga wanachezaje,”amesema.
Simba SC inaanza mazoezi leo baada ya mapumziko ya siku mbili tangu icheze na Stand United Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kutoa sare ya 1-1.
Hiyo ilikuwa ni sare ya tatu mfululizo kikosi cha Kocha Patrick Phiri katika mechi zote tatu za mwanzo za Ligi Kuu, baada ya awali kutoka 2-2 na Coastal Union na 1-1 pia na Polisi Moro.
Sare huzo mfululizo hakika zimewashitua viongozi, benchi la ufundi, wachezaji na hata wapenzi na mashabiki wa Simba, hususan timu ikielekea katika mchezo na mahasimu, Yanga SC Oktoba 18.
Phiri aliyerejea Simba SC Agosti mwaka huu kurithi mikoba ya Mcroatia, Zdravko Logarusic aliyefukuzwa- hadi sasa amekwishaiongoza timu hiyo katika mechi tisa, kati ya hizo akishinda nne kufungwa moja na sare nne.
Jana, kocha wa Yanga SC, Mbrazil Marcio Maximo alikaririwa na BIN ZUBEIRY akisema kwamba hawahofii Simba SC kuelekea mchezo huo- ingawa anawahehimu kama timu nzuri na kongwe.
0 comments:
Post a Comment