Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
SIMBA SC inaweza kuondoka kesho nchini kwenda kuweka kambi Afrika Kusini kwa ajili ya mpambano na mahasimu wao, Yanga SC Oktoba 18, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe yuko Cape Town tangu jana na kikosi kinaweza kuondoka kesho na kurejea Dar es Salaam siku moja kabla ya mechi na watani.
Wacheaji waliopo timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wataondoka Dar es Salaam baada ya mechi na Benin Jumatatu.
Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi hatakwenda kabisa Afrika Kusini kwa sababu atakuwa kwenye majukumu ya kimataifa kwao, Uganda.
Kutwa nzima ya leo, uongozi wa Simba SC ulikuwa unawashughulikia baadhi ya wachezaji ambao hawana pasipoti ili kuhakikisha wanakuwemo kwenye safari kesho.
SIMBA SC inaweza kuondoka kesho nchini kwenda kuweka kambi Afrika Kusini kwa ajili ya mpambano na mahasimu wao, Yanga SC Oktoba 18, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe yuko Cape Town tangu jana na kikosi kinaweza kuondoka kesho na kurejea Dar es Salaam siku moja kabla ya mechi na watani.
Wacheaji waliopo timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wataondoka Dar es Salaam baada ya mechi na Benin Jumatatu.
![]() |
Hans Poppe yuko Cape Town tangu jana na Simba SC inatarajiwa kwenda Afrika Kusini kesho |
Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi hatakwenda kabisa Afrika Kusini kwa sababu atakuwa kwenye majukumu ya kimataifa kwao, Uganda.
Kutwa nzima ya leo, uongozi wa Simba SC ulikuwa unawashughulikia baadhi ya wachezaji ambao hawana pasipoti ili kuhakikisha wanakuwemo kwenye safari kesho.
0 comments:
Post a Comment