IMEWEKWA JUNI 11, 2013 SAA 2:50 USIKU
KIUNGO wa Hispania, Jesus Navas amekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 15 kutoka Sevilla kwenda Manchester City, na kusema Ligi Kuu ya England ni bora kwake kupiga hatua ya maendeleo kama mchezaji.
City imethibitisha dili hilo, na Navas anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na klabu hiyo majira haya ya joto baada ya kiungo wa Shakhtar, Fernandinho aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 30 wiki iliyopita.
Winga huyo wa kulia mwenye umri wa miaka 27 amekamilisha vipimo vya afya Jijini New York, ambako yuko na kikosi cha timu ya taifa ya Hispania kwa maandalizi ya mechi na Ireland na atajiunga na kikosi cha City baada ya Kombe la Mabara.
Wamempata: Claudio Reyna na Navas baada ya Mspanyola huyo kumwaga wino kwenye karatasi za City
Amewasili: Navas amesaini kutoka Sevilla kwa Pauni Milioni 15
Navas hadi sasa ameichezea mechi 23 Hispania, akiisaidia nchi yake kutwaa Kombe la Dunia mwaka 2010 na Euro miaka miwili iliyopita.
Navas alikutana na kiungo wa zamani wa City, Claudio Reyna, aliyechaguliwa hivi karibuni kuwa Mkurugenzi wa Michezo wa New York City FC, Jijini the New York kukamilisha usajili wake.
Mzoefu: Navas ameichezea mechi 23 Hispania, na alishinda mataji ya Kombe la Dunia 2010 na Euro 2012