• HABARI MPYA

    Monday, June 24, 2013

    BAYERN MUNICH WAMTAMBULISHA RASMI PEP KATIKA MKUTANO MZITO LEO ALLIANZ ARENA...JUPP HEYNCCKES ANATIA HURUMA

    IMEWEKWA JUNI 24, 2013 SAA 11:50 JIONI
    WASHINDI wa mataji matatu, Bayern Munich wamemtambulisha kocha wao mpya, Pep Guardiola leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari, The Bavarians wakijiandaa kuendelea kutamba katika soka ya nyumbani na Ulaya.
    Kocha huyo wa zamani wa Barcelona amesema yuko tayari kukabiliana na changamoto za kufundisha timu iliyofanya vizuri msimu uliopita chini ya Jupp Heynckes, ikishinda mataji ya Ligi Kuu ya nyumbani na makombe mawili, pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya.
    "Lazima nikubali mlinganisho," alisema Guardiola, akiwa katika vazi nadhifu la suti ya vipande vitatu ya rangi ya kijivu akizungumza Kijerumani kwenye Mkutano uliofanyika ukumbi wa mikutano wa klabu, Allianz Arena.
    Pressure? Pep Guardiola has just taken over at European champions Bayern Munich
    Shinikizo? Pep Guardiola anakuwa kocha wa mabingwa wapya wa Ulaya, Bayern Munich

    "Lazima niwe tayari kuishi na hiyo. Nipo chini ya shinikizo, wazi, lakini nafahamu hili na nakubali changamoto hii bila woga na ndiyo maana mimi ni kocha,"alisema.
    Guardiola, ambaye aliyeshinda mataji 14 katika miaka minne ya kuwa na Barcelona, usajili wake ni mkubwa Bayern na hasa ikizingatiwa anahamia timu iliyofanya vyema. Alitumia mwaka wake mzima baada ya kuacha kazi Hispania mwaka 2012, kwa kupumzika New York, Marekani.
    "Kitu nachofikiria kwa sasa ni zawadi, baraka kuwa hapa na Bayern,"alisema kocha huyo Mspanyola, aliyesaini Mkataba wa miaka mitatu.
    Confident: And he needs to be - Guardiola has big shoes to fill
    Kujiamini: Guardiola akizungumza leo
    Grand gathering: Many were present to witness Guardiola's unveiling as Bayern boss
    Waliohudhuria mkutano huo wa kutambulishwa Guardiola bosi mpya BayernFabulous four: Guardiola was joined by Matthias Sammer, Karl-Heinz Rummenigge and Uli Hoeness
    Wanne mashuhuri: Guardiola aliungana na Matthias Sammer, Karl-Heinz Rummenigge na Uli Hoeness

    Aisema sababu ya kwanza iliyomfanya akubali ofa ya kuifundisha Bayern ni wachezaji wa klabu hiyo na historia yake.
    Welcome, Pep! The manager already looks comfortable in his surroundings
    Karibu, Pep! Kocha tayari anajisikia nyumbani katikati ya watu
    Big reputation: Guardiola's success at Barcelona means many have high hopes for him in Germany
    Kiroho safi? Guardiola akiwa na kocha anayeondolewa Bayern, Jupp Heynckes. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BAYERN MUNICH WAMTAMBULISHA RASMI PEP KATIKA MKUTANO MZITO LEO ALLIANZ ARENA...JUPP HEYNCCKES ANATIA HURUMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top