• HABARI MPYA

    Tuesday, June 25, 2013

    TEVEZ ATUA JUVE KWA PAUNI MILIONI 10

    IMEWEKWA JUNI 25, 2013 SAA 4:20 USIKU
    MSHAMBULIAJI wa Manchester City, Carlos Tevez anajiandaa kuhamia Juventus baada ya klabu hizo mbili kukubaliana kuuziana mchezaji huyo kwa ada ya Pauni Milioni 10.
    Viongozi wa mabingwa hao wa Serie A walisafiri hadi Uingereza usiku wa jana kukamilisha dili la kumchukua Muargentina huyo.
    Tevez alikaribia kuondoka vibayakipindi cha nyuma City na sasa inatokea ataondoka vizuri Etihad baada ya makubaliano ya kumuuza.
    Oh his way: Carlos Tevez is set to leave England after seven years for Juventus
    Njiani: Carlos Tevez anajiandaa kuondoka England baada ya miaka saba akihamia Juventus

    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amebakiza mwaka mmoja Etihad na anaweza kuondoka bure katika klabu hiyo msimu ujao.
    Tevez anatarajiwa kwenda Turin kufanyiwa vipimo vya afya ili kukamilisha usajili huo.
    Consistent: Tevez has been among Manchester City's key players since his 2009 arrival
    Uhakika: Tevez amekuwa miongoni mwa wachezaji tegemeo wa Manchester City tangu alipowasili mwaka 2009
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: TEVEZ ATUA JUVE KWA PAUNI MILIONI 10 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top