• HABARI MPYA

    Sunday, June 09, 2013

    DORTMUND WAITENGEA MAN UNITED LEWANDOWSKI MLANGONI KABISA BAADA YA KUICHINJIA BAHARINI BAYERN KINOKO

    IMEWEKWA JUNI 9, 2013 SAA 3:40 USIKU
    MTENDAJI Mkuu wa Borussia Dortmund amesema kwamba mshambuliaji Robert Lewandowski hatauzwa kwa Bayern Munich majira haya ya joto.
    Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Poland, mwenye umri wa miaka 24, alisemekana kuhamia timu nyingine Ujerumani, kwa wapinzani wa Dortmund, Bayern lakini sasa Manchester United wanaweza kumnyakua.
    Mchezaji mwenzake Mario Gotze alizua tafrani alipokubali kujiunga na washindi hao wa Ligi Kuu ya Ujerumani kwa msimu ujao na Lewandowski alitarajiwa kumfuata.
    On the move: Robert Lewandowski will not be allowed to sign for Bayern Munich this summer
    Anaondoka: Robert Lewandowski hataruhusiwa kusaini Bayern Munich majira haya ya joto
    CEO wa Dortmund alisema kama ilivyoripotiwa na Bild: "Robert Lewandowski hatahamia FC Bayern mwaka 2013. hiyo ni mwisho. Tumemuambia Robert na wakala wake sasa,".
    United, ambao wanammezea mate Lewandowski kwa muda mrefu, sasa watatazamiwa kupambana kumpata mpachika mabao huyo kama sasa atapenda kuhamia klabu ya nje ya Bundesliga.
    Long-term target: The Poland striker is on Manchester United's transfer wishlist this summer
    Anayetakiwa kwa muda mrefu: Mshambuliaji wa Poland, anatakiwa na Manchester United majira haya ya joto

    Chelsea pia inaweza kuhamishia ndoana zake kwa Lewandowski wakiwa sokoni hivi sasa wanasaka mshambuliaji na kwa sasa wamewalenga Stevan Jovetic, Edinson Cavani na Hulk.
    Bayern Munich's Mario Gomez
    Manchester United's Wayne Rooney
    Wanaondoka: Huku Mario Gomez (kushoto) akitarajiwa kuhama Bayern Munich na Wayne Rooney pia ameripotiwa kutaka kuhama Manchester United, Lewandowski ndiye mbadala wao sahihi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: DORTMUND WAITENGEA MAN UNITED LEWANDOWSKI MLANGONI KABISA BAADA YA KUICHINJIA BAHARINI BAYERN KINOKO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top