KIKOSI cha Simba kimeondoka leo asubuhi kwenda Zambia kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Red Arrows Jumapili Uwanja wa Taifa wa Mashujaa Jijini Lusaka.
Simba SC inahitaji kuulinda ushindi wake wa 3-0 kwenye mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam ili kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kwa mara ya kwanza katika historia yake.
0 comments:
Post a Comment