• HABARI MPYA

    Friday, December 03, 2021

    SIMBA SC WALIVYOIFUATA RED ARROWS LUSAKA


    KIKOSI cha Simba kimeondoka leo asubuhi kwenda Zambia kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Red Arrows Jumapili Uwanja wa Taifa wa Mashujaa Jijini Lusaka.
    Simba SC inahitaji kuulinda ushindi wake wa 3-0 kwenye mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam ili kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kwa mara ya kwanza katika historia yake.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC WALIVYOIFUATA RED ARROWS LUSAKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top