• HABARI MPYA

    Saturday, December 04, 2021

    POLISI TANZANIA YAICHAPA TANZANIA PRISONS 1-0


    BAO la Tariq Simba dakika ya tano ya muda wa nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida limeipa Polisi Tanzania ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
    Polisi Tanzania inafikisha pointi 14 na kurejea nafasi ya tatu, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake katika nafasi ya 12 kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi nane sasa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: POLISI TANZANIA YAICHAPA TANZANIA PRISONS 1-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top