• HABARI MPYA

    Friday, March 25, 2016

    MASHABIKI WAIPOKEA KWA 'VISINGELI' STARS

    Mashabiki wa kikundi cha kuisapoti Taifa Stars wakicheza kwa usiku wa manane jana Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam wakati wa kuipokea timu yao ya taifa ikirejea kutoka Chad ambako Jumatano iliwafunga wenyeji 1-0 katika mchezo wa kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika 2017
    Mashabiki walicheza ngoma zao kwa furaha kupongeza wachezaji na timu
    Wake kwa waume walijitokeza Uwanja wa Ndege usiku wa jana kuipokea Taifa Stars kwa furaha
    Katikati ni mwigizaji nyota, Dk Cheni akiwa na mmoja wa viongozi wa kikundi cha kuisapoti Taifa Stars, Papa Ziota (kushoto)
    Hadi ma- ustadh walikuwepo jana Uwanja wa ndege kuipokea Taifa Stars ya Tanzania
    Akina mama hawa waliwaacha waume zao vitandani kwa ajili ya Taifa Stars
    Vijana nao hawakuwa nyuma katika mapokezi hayo, waliacha starehe zote za kipindi hiki cha kuelekea Pasaka

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MASHABIKI WAIPOKEA KWA 'VISINGELI' STARS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top