KLABU ya Manchester United imefanikiwa kushinda mbio za kuwania saini ya Memphis Depay baada ya mchezaji huyo na wakala wake kufanya mazungumzo mazuri na Louis van Gaal kuhusu uhamisho wa Pauni Milioni 25.
Klabu hiyo imethibitisha uhamisho huo leo na Depay atajiunga na United - iwapo akifaulu vipimo vya afya dirisha la usajili litakapofunguliwa Juni.
United imesema kupitia ukurasa wake Twitter: 'Manchester United imefikia makubaliano na PSV Eindhoven na Memphis Depay kwa uhamisho wa mchezaji huyo, iwapo akifaulu vipimo vya afya,".
Winga wa PSV Eindhoven, Depay akisherehekea na taji la Ligi Kuu Uholanzi, maarufu kama Eredivisie mwezi uliopita
"Itategemea na kama atafaulu vipimo vya afya, mpango utakamailishwa mara dirisha la usajili litakapofunguliwa mwezi Juni.'
Kocha wa PSV, Philip Cocu ametangaza hatua ya kikosi chake asubuhi ya Alhamisi.
Mkurugenzi wa Usajili, Marcel Brands amesemea kupitia tovuti ya PSV; "Tunajivunia sana juu ya uhamisho huu ujao. Memphis ametokea kwenye mpango wa soka ya vijana katika akademi ya PSV na ametoa mchango mkubwa kwa timu kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Uholanzi msimu huu.
Depay akishangilia na taji la Eredivisie na kulia akiichezea Uholanzi katika Kombe la Dunia


.png)
0 comments:
Post a Comment