Mwanasoka wa kimataifa wa Argentina, Sergio 'Kun' Aguero akishangilia baada ya kufunga bao lake la 22 katika Ligi Kuu England msimu huu katika ushindi wa 1-0 wa Manchester City dhidi ya Tottenham Uwanja wa White Hart Lane usiku huu.
Bao la Aguero linaifanya City ifikishe pointi 70 baada ya kucheza mechi 35, ikiendelea kukamata nafasi ya pili, nyuma ya Chelsea waliojihakikishia ubingwa leo kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Crystal Palace leo kwa kufikisha pointi 83 baada ya kucheza mechi 35. City ndiyo waliokuwa mabingwa watetezi na sasa wanapambana na Arsenal na Manchester United kuwania nafasi ya pili.
PICHA ZAIDI NENDA:
http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-3066327/Tottenham-0-1-Manchester-City-Sergio-Aguero-strikes-goal-game-earn-victory-Manuel-Pellegrini-s-men.html#ixzz3Z64Osai9
0 comments:
Post a Comment