• HABARI MPYA

    Friday, May 08, 2015

    HALI YA PELE SASA SHWARI, HOSPITALI YATHIBITISHA

    ZOEZI la upasuaji wa gwiji wa soka Brazil, Pele mwenye umri wa miaka 74, limemalizika salama na anaendelea vizuri kwa sasa. Taarifa ya hospitali ya Albert Einstein mjini Sao Paulo, Brazil imethibitisha Pele kwa sasa yuko vizuri baada ya upasuaji huo. 
    Pele alifanyiwa upasuaji Jumanne wa malazi ya nyama za mdomoni zinazoshikilia meno, ambayo tovuti hiyo imesema yanaongeza hatari ya ugonjwa wake wa kibovu cha mkojo.
    Pele, ambaye jina lake halisi ni Edson Arantes do Nascimento, aliruhusiwa kutoka katika hospitali hiyo hiyo mapema Desemba baada ya kulazwa kwa wiki mbili kwa matatizo hayo hayo.
    Three-time World Cup winning Brazil striker Pele has undergone successful prostate surgery 
    Pele anaendelea vizuri kiafya baada ya kufanyiwa upasuaji

    Mshindi huyo wa mataji matatu ya Kombe la Dunia akiwa na Brazil bado hajatokea hadharani kuzungumzia afya yake.
    Akiwa amefunga mabao zaidi ya 1,280 jumla enzi zake anacheza soka, Pele anapewa heshima na mashabki wengi kama mchezaji bora zaidi daima wa dunia kuahi kutokea duniani.
    Pele exchanges shirts with former Argentina forward Diego Maradona (left) at an event back in 2005
    Pele akibadilishana jezi na mshambuliaji wa zamani wa Argentina, Diego Maradona (kushoto) mwaka 2005
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HALI YA PELE SASA SHWARI, HOSPITALI YATHIBITISHA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top