KLABU ya Paris Saint-Germain inamtaka kwa mkopo winga ambaye hafanyi vizuri Manchester United, Angel di Maria wakiamini wanaweza kupewa baada ya Mashetani hai Wekundu kumpata winga wa PSV, Memphis Depay.
Di Maria alitua Old Trafford kwa dau la rekodi Pauni Milioni 60 kutoka Real Madrid msimu huu, lakini amejikuta katika mwanzo mgumu Ligi Kuu ya England.
Na ripoti nchini Ufaransa zinasema kwamba PSG wapo tayari kumpa nafasi Di Maria afufue makali baada ya kukwama England.
Angel di Maria alitua Manchester United msimu huu kutoka Real Madrid kwa dau la rekodi Pauni Milioni 60


.png)
0 comments:
Post a Comment