// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SIMBA SC NA KCCA NUSU FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI YANGA NA AZAM AU MTIBWA SUGAR - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SIMBA SC NA KCCA NUSU FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI YANGA NA AZAM AU MTIBWA SUGAR - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, January 06, 2015

    SIMBA SC NA KCCA NUSU FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI YANGA NA AZAM AU MTIBWA SUGAR

    Na Mahmoud Zubeiry, ZANZIBAR
    VIGOGO wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC, Mtibwa Sugar, Simba na mahasimu wao, Yanga SC wamekwenda wote Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi, huku kukiwa kuna uwezekano wa kukutana baina yao katika Nusu Fainali.
    Robo Fainali ya kwanza itachezwa kesho Saa 2:15 Usiku Uwanja wa Amaan, kati ya Simba SC na Taifa ya Jang’ombe, wakati keshokutwa Yanga SC itamenyana na JKU, mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya KCCA na Polisi Saa 9:00 Alasiri, Azam FC na Mtibwa Sugar Saa 11:00.

    Simba SC inaweza kukutana na KCCA ya Uganda katika Nusu Fainali ya Kombe la Mapindzi Januari 10, mwaka huu

    MATOKEO NA RATIBA KOMBE LA MAPINDUZI 

    Jan 1, 2015:
    JKU 2-0 Mafunzo
    Polisi 1-0 Shaba
    Simba 0-1 Mtibwa Sugar
    Jan 2, 2015
    KMKM 0-0 Mtende
    KCCA 2-2 Azam FC
    Yanga SC 4-0 Taifa 
    Jan 3, 2015;
    JKU 1-1 Mtibwa Sugar 
    Mafunzo 0-1 Simba SC
    Jan 4, 2015
    KCCA 3-0 Mtende
    KMKM 0-1 Azam FC
    Taifa 1-0 Shaba
    Yanga 4-0 Polisi
    Jan 5, 2015
    Mtibwa Sugar 0-0 Mafunzo
    Simba SC 1-0 JKU
    Jan 6, 2015;
    KCCA 2-1 KMKM
    Azam FC 1-0 Mtende
    Polisi 0-0 Taifa Jang’ombe
    Yanga 1-0 Shaba
    ROBO FAINALI
    Jan 7, 2015
    Simba Vs Taifa 2:15 Usiku
    Jan 8 2015
    KCCA Vs Polisi 9:00 Alasiri
    Azam Vs Mtibwa 11:00Jioni
    Yanga  Vs JKU  2:15 Usiku
    NUSU FAINALI
    Jan 10, 2015
    Simba/Taifa Vs KCCA/Polisi Saa 10:00 jioni
    Azam/Mtibwa Vs Yanga/ JKU Saa 2:15 usiku
    FAINALI
    Jan 13, 2015
    Kwa mujibu wa Ratiba ya mashindano haya, Nusu Fainali zitachezwa Januari 10 Uwanja wa Amaan, ambazo zitawakutanisha mshindi kati ya Simba na Taifa dhidi ya mshindi kati ya KCCA ya Uganda na Polisi Zanzibar na mshindi kati ya Azam FC na Mtibwa Sugar dhidi ya mshindi kati ya Yanga na JKU.
    Simba SC inapewa nafasi kubwa ya kuitoa Taifa na KCCA inapewa nafasi kubwa ya kuitoa Polisi- hivyo kuna uwezekano timu hizo zilizokutana katika Fainali mwaka jana, zikakutana katika Nusu Fainali mwaka huu. 
    Yanga SC inapewa nafasi ya kuitoa JKU, wakati mchezo kati ya Azam FC na Mtibwa Sugar, lolote linaweza kutokea. 
    Kwa vyovyote, uhondo wa Kombe la Mapinduzi unaanza kesho wakati wa Robo Fainali, Simba SC ikimenyana na Taifa, ambayo walikutana nayo katika mchezo wa kirafiki na kushinda 3-1 Uwanja wa Amaan. 
    Hatua ya makundi ya michuano hiyo imefikia tamati leo mchezo wa mwisho wa Kundi A, kati ya Yanga SC na Shaba Uwanja wa Amaan usiku huu. Yanga SC, imeshinda 1-0 bao pekee la winga Mbrazil, Andrey Coutinho dakika ya 86.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC NA KCCA NUSU FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI YANGA NA AZAM AU MTIBWA SUGAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top