AIBU. Borussia Dortmund wameitandika Bayern Munich mabao 3-0 katika Bundesliga usiku huu tena kwenye Uwanja wao wa nyumbani, Allianz Arena.
Ni mabao ya Henrikh Mkhitaryan, Marco Reus na Jonas Hofmann yaliyomtoa machozi kocha Pep Guardiola mbele ya timu ya Jurgen Klopp.
Bayern tayari ni mabingwa Bundesliga na wametinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wakati Dortmund imejihakikishia kucheza michuano hiyo mikubwa ya Ulaya mwakani licha ya kutolewa na Real Madrid katika michuano ya mwaka huu wiki hii katika Robo Fainali.
Shapu shuta: Nyota wa Dortmund, Henrikh Mkhitaryan akifunga bao pekee dhidi ya Bayern Munich
0 comments:
Post a Comment