IMEWEKWA MEI 16, 2013 SAA 6:30 USIKU
MSHAMBULIAJI Mario Balotelli hastaajabu Roberto Mancini kufukuzwa Manchester City kwa sababu ya matatizo ya kocha wake huyo wa zamani na klabu hiyo.
Balotelli, ambaye alisajiliwa na Mancini City kabla ya kuuzwa AC Milan Januari, amesema Mtaliano mwenzake huyo ni bonge la kocha.
Mancini alifukuzwa City Jumatatu baada ya timu kushindwa kufikia malengo yaliyotarajiwa na wamiliki na sasa nafasi yake inatarajiwa kuzibwa na Manuel Pellegrini wa Malaga.
Angalia video chini
Sacked: But Roberto Mancini, according to Mario Balotelli, is a great manager
Champions: Balotelli (left) and Mancini (centre) at City last May
Alipoulizwa kuhusu kufukuzwa kwa Mancini, Balotelli aliiambia CNN: "Sishangai kabisa, lakini wakati nilipokuwa naye, alikuwa kocha babu kubwa na tulikuwa na moja ya timu nzuri kati ya nilizowahi kuchezea, wachezaji wazuri.
"Sijui kwa nini hakushinda (taji). Lakini dhahiri kulikuwa kuna matatizo ya ndani. Nipo hapa (Milan) hivyo sifahamu,".
Ndondi: Balotelli na Mancini wakikwidana enzi zao Manchester City