• HABARI MPYA

    Wednesday, May 22, 2013

    MOURINHO KUISUKA UPYA SAFU YA ULINZI CHELSEA...NA ATAANZA NA LUIZ

    IMEWEKWA MEI 22, 2013 SAA 12:45
    KLABU za Real Madrid na Barcelona zinamtaka beki wa kati wa Chelsea, David Luiz.
    Mbrazil huyo anaweza kuwa lulu mbele ya kocha mpya anayekuja, Jose Mourinho ambaye amevutiwa na uwezo wake katika nafasi ya ulinzi.
    Luiz aliigharimu Chelsea Pauni Milioni 21 nna watataka faida ikibidi kuuuza bidhaa hiyo waliyoinunua mwaka 2011.
    Character: Chelsea defender David Luiz signed for £21m from Benfica
    Mpiganaji: Beki wa Chelsea, David Luiz alisajiliwa kwa Pauni Milioni 21 kutoka Benfica
    Star: Luiz was an integral part to Chelsea' Europa League triumph
    Nyota: Luiz alikuwa na mchango mkubwa wakati Chelsea inatwaa Europa League

    Mourinho anataka beki mpya wa kati, kiungo mkabaji na angalau mshambuliaji mmoja katika kurejea kwake Stamford Bridge. Luiz amekuwa akitumika kama kiungo mkabaji chini ya Rafa Benitez na imemsaidia kupunguza makosa yake wakati anacheza kama beki.
    Chelsea imeonyesha nia ya kumsajili mchezaji anayetakiwa na Liverpool, Krygiakos Papadopoulos wa Schalke, lakini inamchukulia kinda huyo wa miaka 21 kama ghali sana. Mourinho ni shabiki mkubwa wa Raphael Varane wa Real Madrid pia, lakini suala hilo litaingiliwa na siasa zake za kuondoka Bernabeu. 
    Tayari, wanaonekana kuimarisha safu yao ya ulinzi wakiwa na Branislav Ivanovic ambaye pia anawezwa kuhamishiwa beki ya kulia.
    Talent: Madrid's Raphael Varane (heading) has left a significant impact on Mourinho
    Kipaji: Raphael Varane wa Real Madrid (akipiga juu) anakubalika mno mbele ya Mourinho
    Clean sheets: Jose Mourinho's first job at Chelsea would be to strengthen their defence
    Kazi ya kwanza ya Jose Mourinho Chelsea itakuwa kuimarisha safu ya ulinzi

    Madrid itakijenga upya kikosi cha Mourinho kupitia kwa Carlo Ancelotti. Watakuwa tayari kumuuza beki Pepe kuliko Varane na Manchester City wamepewa ofa ya kumsajili beki huyo Mreno kwa Pauni Milioni 20.
    Kwa upande wao, Barcelona wanapambana kuwania saini ya beki wa kati ambaye hatazidi Pauni Milioni 25. Luiz yumo kwenye orodha yao muda mrefu, lakini si kipaumbele cha mwanzoni.
    Tough: Mourinho will have to decide on the futures of John Terry and Frank Lampard during next season
    Mourinho atatakiwa kuamua mustakabali wa John Terry na Frank Lampard msimu ujao

    Walimtaka Thiago Silva kutoka Paris St Germain, lakini ni ghali mno wakati Manchester City hawako tayari kumuuza Vincent Kompany. Barca inamtaka beki kinda wa Roma, Marquinhos lakini anaweza kuwa tayari kubaki kwa msimu mwingine Italia.
    Thomas Vermaelen wa Arsenal anaweza kurejesha makali yake, lakini kumaliza kwake msimu vibaya kunamfanya Luiz awe midomoni mwa watu zaidi yake.
    Vincent Kompany
    Thiago Silva
    Vincent Kompany kushoto na Thiago Silva kulia
    Scouted: But Arsenal sub Thomas Vermaelen is being watched by Chelsea
    Thomas Vermaelen amekuwa akimulikwa na Chelsea
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MOURINHO KUISUKA UPYA SAFU YA ULINZI CHELSEA...NA ATAANZA NA LUIZ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top