• HABARI MPYA

    Tuesday, May 21, 2013

    YANGA SC WAPANGWA KUNDI C LAINI KAGAME, SIMBA KUNDI A LA HATARI TUPU

    Mabingwa watetezi; Yanga SC wamepangwa Kundi C

    Na Mahmoud Zubeiry, IMEWEKWA MEI 21, 2013
    SAA 4:00 USIKU
    BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) limewapanga katika Kundi C, mabingwa watetezi, Yanga SC katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati, Kombe la Kagame leo katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Juni 18 hadi Julai 2, mwaka huu mjini Khartoum, Sudan.
    Katika kundi hilo, mabingwa hao mara mbili mfululizo wa taji hilo wamepangwa na Ports ya Djibouti, Express ya Uganda na  Vital 'O'  ya Burundi, wakati wapinzani wao wa jadi, Simba SC wamepangwa kundi A pamoja na wenyeji El-Mereikh, Elman  ya Somalia na APR ya Rwanda
    Mabingwa wa Kenya, Tusker wamepangwa Kundi B pamoja na wenyeji wengine, Al-Hilal, Al Ahly Shandy ya Sudan, Falcons ya Zanzibar na Al-Nasir Juba ya Sudan Kusini.
    Yanga itaanza kampeni zake Juni 20 kwa kumenyana na Express na Simba SC itashuka dimbani Juni 21 kufungua dimba na El-Mereikh, mechi zote zikichezwa Elfashar.
    Katibu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesema zawadi za washindi zimeongezeka kutoka dola za Kimarekani 60,000 anazotoa Rais wa Rwanda, Paul Kagame hadi dola 80,000 baada ya Mwenyekiti wa Yanga SC, Yussuf Manji kuongeza dola 20,000.
    Lakini Musonye amesema wanataka zawadi za washindi ziwe jumla dola 100,000 hivyo wanatafuta fedha za kuongezea. 
    Wawakilishi; Simba SC wapo Kundi A la kifo


    KUNDI A: El-Merrekh -(Sudan), APR (Rwanda), 
    Simba SC (Tanzania), Elman (Somalia) - EL FASHER
    KUNDI B: Al-Hillal (Sudan), Tusker (Kenya), Al Nasri (Sudan Kusini), Falcon (Zanzibar),  Al Shandy (Sudan) - KADUGLI
    KUNDI C: Yanga SC (Tanzania), Express (Uganda), Ports (Djibout), Vitaloo (Burundi) - EL FASHIR

    RATIBA KOMBE LA KAGAME KUANZIA JUNI 18 HADI JULAI 2, 2013 (EL-FASHIR NA KADUGLI - SUDAN)
    TAREHETIMUTIMUKUNDI/MUDAUWANJA
    18.06.2013.TUSKER SUPER FALCON B - SAA 8:00 MCHANAKADUGLI
    AL HILLAL AL NASRI B -SAA 10:00 JIONIKADUGLI
    19.06.2013.VITALOOPORTS  C - SAA 10:00 JIONIEL-FASHER
    20.06.2013.YANGA SC EXPRESS C - SAA 8:00 MCHANAEL-FASHER
    20.06.2013.ELMAN FC APR FC A - SAA 10:00 JIONIEL-FASHER
    20.06.2013.SUPER FALCON AL NASRI B -SAA 8:00 MCHANAKADUGLI
    20.06.2013.TUSKER AL-SHANDY B -SAA 10:00 JIONIKADUGLI
    21.06.2013.EL MERREIKH SIMBA SC A -SAA 10:00 JIONIKADUGLI
    22.06.2013.EXPRESS FC VITALOO C - SAA 8:00 MCHANAEL-FASHER
    PORTS YANGA SC C -SAA 10:00 JIONIEL FASHER
    22.06.2013.AL NASRITUSKER B - SAA 8:00 MCHANAKADUGLI
    AL SHANDY AL HILAL B -SAA 10:00 JIONIKADUGLI
    23.06.2013APR SIMBA SC A - SAA 8:00 MCHANAEL-FASHER
    EL MERREIKH  ELAM FC A -SAA 10:00 JIONI
    EL-FASHER
    24.06.2013AL NASRI AL SHANDY B -SAA 8:00 MCHANAKADUGLI
    SUPER FALCON AL HILLAL B -SAA 10:00 JIONIKADUGLI
    24.06.2013. PORTSEXPRESS FC C -SAA 10:00 JIONIEL-FASHER
    25.06.2013.VITALOO YANGA SC C -SAA 10:00 JIONIEL-FASHER
    26.06.2013.AL SHANDY SUPER FALCON B -SAA 8:00 MCHANAKADUGLI
    AL HILLAL TUSKER B -SAA 10:00 JIONIKADUGLI
    26.06.2012.SIMBA SC ELMAN FC A -SAA 8:00 MCHANAEL-FASHER
    APR FC EL MERREIK A -SAA 10:00 JIONIEL-FASHER
    27.06.2013.MAPUMZIKOMAPUMZIKOMAPUMZIKO
      MAPUMZIKO
    28.06.2013.(23) B2 VS C2(24) B1 VS BEST QUTATANGAZWAKADUGLI
    28.06.2013.(25) C1 VS A2(26) A1 VS B3UTATANGAZWAEL-FASHER
    30.06.2013.WNR 23 VS WNR 25WIN 24 VS WIN 26UTATANGAZWA
    01.07.2013.MAPUMZIKOMAPUMZIKOMAPUMZIKOMAPUMZIKO
    02.07.2013.ILIYOFUNGWAILIYOFUNGWAMSINDI WA TATUEL-FASHER
     ALIYESHINDA 27 ALIYESHINDA 28  FAINALI EL-FASHER
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA SC WAPANGWA KUNDI C LAINI KAGAME, SIMBA KUNDI A LA HATARI TUPU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top