• HABARI MPYA

    Sunday, May 19, 2013

    USHINDI KAMA WA JANA HAUJATOKEA YANGA TANGU MWAKA 2000 MABAO YA IDDI MOSHI AKITOKEA FUNGATE

    Didier Kavumbangu kulia na Haruna Niyonzima kushoto wakimdhibiti Mrisho Ngassa katikati

    Na Mahmoud Zubeiry, IMEWEKWA MEI 19, 2013 SAA 4:50 ASUBUHI
    USHINDI wa mabao 2-0 kwa Yanga SC jana dhidi ya wapinzani wao wa jadi, Simba SC ndio mnono zaidi kwao dhidi ya mahasimu wao hao, ndani ya miaka 13 katika Ligi Kuu na miaka 10 kwa ujumla.
    Yanga SC jana iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Simba SC, yaliyotiwa kimiani na Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza moja kila kipindi.
    Kabla ya hapo, mara ya mwisho katika Ligi Kuu Yanga kushinda kwa tofauti ya mabao mawili dhidi ya Simba SC, ilikuwa ni Agosti 5, mwaka 2000, wakati mabao ya Iddi Moshi Shaaban yalipoipa timu hiyo ushindi wa 2-0.
    Baada ya hapo, Yanga iliuja kupata ushindi mzuri zaidi dhidi ya Simba SC Aprili 20, mwaka 2003 Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza 3-0 katika mchezo wa kirafiki uliondaliwa na Dika Sharp, mabao yakifungwa na Kudra Omary dakika ya 30, Heri Morris dakika ya 32 na Salum Athumani dakika ya 47.
    Tofauti na hapo, Yanga imekuwa ikishinda 1-0 na 2-1 dhidi ya watani wao hao kwa kipindi chote hicho na zaidi ni wao ndiyo wamekuwa wakitoka vichwa chini mara nyingi baada ya mechi za watani. 
    Je, 2-0 za jana ni mwanzo wa zama mpya za ubabe wa Yanga kwa Simba?
    Mchezaji bora wa mechi ya jana, Athumani Iddi 'Chuji' akimiliki mpira ya Athumani Iddi 'Chuji'

    REKODI YA SIMBA NA YANGA LIGI KUU TANGU 2000:
    AGOSTI 5, 2000
    Yanga v Simba,  
    2-0, Uhuru (Dar)
    MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. 
    (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)

    SEPTEMBA 1, 2001
    Simba v Yanga 
    1-0, Uhuru (Dar)
    MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76

    SEPTEMBA 30, 2001
    Simba v Yanga 
    1-1, Kirumba (Mwanza)
    WAFUNGAJI: 
    Simba: Joseph Kaniki dk. 65, 
    Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86

    AGOSTI 18, 2002
    Simba v Yanga 
    1-1, Uhuru, (Dar)
    WAFUNGAJI: 
    Simba: Madaraka Selemani 65
    Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89

    NOVEMBA 10, 2002
    Simba v Yanga 
    0-0, Uhuru (Dar)

    SEPTEMBA 28, 2003
    Simba v Yanga 
    2-2, Uhuru (Dar) 
    WAFUNGAJI: 
    Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
    Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55

    NOVEMBA 2, 2003
    Simba v Yanga 
    0-0, Uhuru (Dar)

    AGOSTI 7, 2004
    Simba v Yanga 
    2-1, Uhuru (Dar)
    WAFUNGAJI: 
    Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
    Yanga: Pitchou Kongo dk. 48

    SEPTEMBA 18, 2004
    Simba v Yanga 
    1-0, Uhuru (Dar)
    MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82

    APRILI 17,  2005
    Simba v Yanga
    2-1, Jamhuri (Moro)
    WAFUNGAJI: 
    Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
    Yanga: Aaron Nyanda dk. 39

    AGOSTI 21, 2005
    Simba v Yanga 
    2-0, S.A. Abeid (Arusha)
    MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56

    MACHI 26, 2006 
    Simba v Yanga.
    0-0, Uhuru (Dar)

    OKTOBA 29, 2006
    Simba v Yanga
    0-0, Uhuru, (Dar)

    JULAI 8, 2007
    Simba v Yanga
    1-1, Jamhuri (Moro)
    WAFUNGAJI:
    Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
    Yanga: Said Maulid (dk. 55).
    (Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo 1-1 dakika 120).

    OKTOBA 24, 2007:
    Simba Vs Yanga 
    1-0, Jamhuri (Moro) 
    Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe

    APRILI 27, 2008:
    Simba Vs Yanga
    0-0, Uhuru (Dar) 

    OKT 26, 2008
    Yanga Vs Simba
    1-0, Taifa (Dar)
    MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15. 

    APRILI  19, 2009
    Simba Vs Yanga 
    2-2, Taifa (Dar)
    WAFUNGAJI:
    SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
    YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90

    OKTOBA 31, 2009
    Simba Vs Yanga
    1-0, Taifa (Dar)
    MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26

    APRILI 18, 2010
    Simba Vs Yanga
    4-3, Taifa (Dar)
    WAFUNGAJI:
    SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+  
    YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89 

    OKTOBA 16, 2010:
    Yanga Vs Simba
    1-0, Kirumba, Mwanza
    MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70

    MACHI 5, 2011
    Simba Vs Yanga
    1-1, Taifa (Dar)
    WAFUNGAJI:
    YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59. 
    SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.
    (Refa Orden Mbaga alizua tafrani uwanjani, kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidia wake namba moja)

    OKTOBA 29, 2011
    Yanga Vs Simba
    1-0, Taifa (Dar)
    MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75

    MEI 6, 2012
    Simba Vs Yanga SC
    5-0, Taifa (Dar), 
    WAFUNGAJI: 
    Emmanuel Okwi (dk 2 na 62), Felix Sunzu (penalti 56), Juma Kaseja (penalti dk 67) na Patrick Mafisango (penalti dk 72)

    OKTOBA 3, 2013
    Simba Vs Yanga SC
    1-1, Taifa (Dar)
    WAFUNGAJI:
    Simba SC: Amri Kiemba dk3
    Yanga SC: Said Bahanuzi dk65
    (Ligi Kuu)

    MEI 18, 2013
    Yanga Vs Simba SC
    2-0, Taifa (Dar)
    WAFUNGAJI: Didier Kavumbangu dk 5 na Hamisi Kiiza dk 62.
    Mashabiki wa Yanga jana

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: USHINDI KAMA WA JANA HAUJATOKEA YANGA TANGU MWAKA 2000 MABAO YA IDDI MOSHI AKITOKEA FUNGATE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top