• HABARI MPYA

    Sunday, May 26, 2013

    NEYMAR AIKATAA REAL MADRID, KUSAINI MIAKA TANO NA BARCELONA KESHO


    IMEWEKWA MEI 26, 2013 SAA 1:00 ASUBUHI
    MABINGWA wa Hispania, Barcelona wamekubali kumsajili mshambuliaji wa Brazil, Neymar kutoka klabu ya Santos.
    Nyota huyo mwenye umri wa miaka 21, atasaini mkataba wa miaka mitano, klabu hiyo imesema na mchezaji mwenyewe amethibitisha atasaini kesho.
    Taarifa ya Barcelona imesema: "FC Barcelona na Santos zimekubaliana kuhusu Neymar da Silva Santos Junior. Mshambuliaji wa Kibrazil atakuwa mchezaji wa Blaugrana  kwa miaka mitano ijayo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 ni miongoni mwa wachezaji wanaochipukia vizuri duniani.'
    Heading off: Neymar left a heartfelt message for the fans of FC Santos
    Anaondoka: Neymar anaondoka na chini ni ujumbe alioandika kwa ajili ya mashabiki wa FC Santos
    Neymar's message

    Neymar alilazimika kuamua mustakabali wake, baada ya klabu yake, Santos kusema Ijumaa kwamba wamepokea ofa mbili kwa ajili ya nyota huyo na Barca ikathibitika kuwa ni moja ya klabi zilizotoa ofa huku, Real Madrid ikidhaniwa kuwa ni klabu nyingine.
    Neymar am,ethibitisha uamuzi wake kwa kuandika kwenye Instagram: "Nipo hapa na marafiki na familia na wananisaidia kuandika vitu vichache hapa. Siwezi kusema hadi Jumatatu. Familia yangu na rafiki zangu tayari wanajua uamuzi wangu.
    Jumatatu nitasaini mkataba na Barcelona,".'
    Mkataba wake na Santos unatarajiwa kumalizika msimu ujao na baadhi ya taarifa zinasema kwamba makubaliano na Barcelona yalifikiwa mwaka mmoja uliopita.
    Neymar atawaaga mashabiki wa Santos katika mchezo wa leo wa ufunguzi wa msimu dhidi ya Flamengo.
    Home hero: Neymar (right) has spent his whole career at Santos and has won 32 caps for his country
    Anafuata nyayo: Neymar (kulia) amekuwa akiichezea Santos muda wote na ameichezea timu ya taifa ya Brazil mechi 32. Hapa yupo na Mwanasoka Bora wa zamani wa dunia, Mbrazil mwenzake, Ronaldinho, aliyewahi kung'ara Barcelona.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NEYMAR AIKATAA REAL MADRID, KUSAINI MIAKA TANO NA BARCELONA KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top