• HABARI MPYA

    Tuesday, May 28, 2013

    KIMENUKAAA; RAIS REAL MADRID AAHIDI KUMPA CHOCHOTE RONALDO ILI MRADI ABAKI BERNABEU...KWANZA, ATAMFANYA CRISTIANO AWE MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI


    IMEWEKWA MEI 28, 2013 SAA 11:00 JIONI
    RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez anajiandaa kumfanya Cristiano Ronaldo awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani katika jithada za kumshawishi abaki Bernabeu, baada ya kuondoka kwa Jose Mourinho.
    Perez amesema: "Ningependa Cristiano Ronaldo awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani. Tunakwenda kufanya kila kitu katika mikono yetu kumfanya awe na furaha.’
    Nyota huyo wa zamani wa Manchester United amekuwa akihusishwa na uvumi wa kurejea Old Trafford msimu ujao au kwenda kujiunga na Matajiri wa Ufaransa, Paris Saint-Germain - lakini Perez anapambana kumzuia Madrid kwa muda zaidi. 
    Bumper deal: Perez is prepared to break the bank to keep Ronaldo at Real
    Dili kweli: Perez anajiandaa kubomoa benki ili Ronaldo abaki Real
    Star man: Ronaldo had another fine season despite Real not winning a major trophy
    Nyota kweli: Ronaldo alikuwa na msimu mwingine mzuri Real licha ya kutoshinda taji lolote
    Unhappy: Ronaldo is thought be considering a move away from the Spanish capital
    Hana furaha: Ronaldo inasadikiwa anataka kuondoka Hispania

    Ronaldo amekuwa mchezaji mkubwa duniani tangu anunuliwe kwa Pauni Milioni 80 kutua Hispania mwaka 2009, akifunga mabao 146 katika mechi 135.
    Rais wa Madrid pia amesema kwamba licha ya matatizo yote yaliyotokea na Special One msimu huu, wachezaji bao wanamzungumzia vizuri Mourinho.
    Alisema: "Wachezaji wanamzungumzia vizuri tu Mourinho. Wameniambia alikuwa bora. Hatujui nani atakuwa kocha mpya. Tutazungumzia hilo wiki ijayo. Lakini tunataka Zinedine Zidane awe kiongozi wa mpango huu,"alisema.
    Kazi ya kwanza ya Zidane ni kuhakikisha anamsajili nyota wa Tottenham, Gareth Bale kwa Pauni Milioni 65.
    Power-brokers: Perez (above) and Zidane (below) want to unite Ronaldo and Bale at the Bernabeu
    Rais wa Real, Perez anataka Ronaldo abaki na Bale atue Bernabeu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KIMENUKAAA; RAIS REAL MADRID AAHIDI KUMPA CHOCHOTE RONALDO ILI MRADI ABAKI BERNABEU...KWANZA, ATAMFANYA CRISTIANO AWE MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top