![]() |
| Kocha wa timu ya taifa ya DRC, Le Roy akizungumza na wachezaji wa U-20 ya TPM |
KIKOSI cha timu ya vijana chini
ya umri wa miaka 20 cha Tout Puissant Mazembe kinaendelea na maandalizi ya
ziara yao ya Ulaya baada ya Jumapili kuifunga Ravens 4-1 kwenye Uwanja mpya wa Lubumbashi
Sport Kamalondo.
Mabao ya Maisha, Ushindi (mawili)
na Nasri yaliipa ushindi U-20 ya TPM mbele ya macho ya kocha wa timu ya taifa
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Claude Le Roy.
Waandaaji wa michuano itakayofanyika
Uswisi na Ujerumani wamekwishatoa ratiba na inafahamika U20 ya TPM itacheza na
timu gani.
Michuano hiyo iliyopewa jina Blue
Star Cup, mjini Zurich Jumatano ya Mei 16, saa 9:30 kwa saa za huko, Mazembe itacheza
na wenyeji FC Blue Stars na siku hiyo hiyo saa 12:30 itacheza na Borussia
Moenchengladbach.
Alhamisi ya Mei 17, saa 3:15
asubuhi, Mazembe itacheza na Grasshopper
Club Zurich na saa 4:50 itacheza na Panathinaikos.
Klabu sita Afrika zimepeleka
timu zao za vijana kwenye michuano hiyo ya FIFA Blue Stars, ambazo na TPM,
nyingine ni Al Ahly ya Cairo, Nania FC na Dwarfs za Ghana, Abuja Boys ya Nigeri
na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
Jumamosi ya Mei 26, saa 8:45
litafanyika gwaride rasmi la utambulisho wa timu katika ufunguzi wa michuano
hiyo.
Saa 10.50: Mazembe itacheza na FSV
Mainz 05, Jumapili ya Mei 27, saa 12:45, Mazembe itacheza na TUS Ergenzingen na
saa 11:55 Mazembe itacheza na timu ya
taifa ya U-19 ya Bulgaria wakati Mei 28, saa 4:00 fainali zitaanza.



.png)
0 comments:
Post a Comment