• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    TIMU LA KINA SAMATTA LAENDA MASHINDANONI ULAYA

    Kocha wa timu ya taifa ya DRC, Le Roy akizungumza na wachezaji wa U-20 ya TPM
    KIKOSI cha timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 cha Tout Puissant Mazembe kinaendelea na maandalizi ya ziara yao ya Ulaya baada ya Jumapili kuifunga Ravens 4-1 kwenye Uwanja mpya wa Lubumbashi Sport Kamalondo.
    Mabao ya Maisha, Ushindi (mawili) na Nasri yaliipa ushindi U-20 ya TPM mbele ya macho ya kocha wa timu ya taifa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Claude Le Roy.
    Waandaaji wa michuano itakayofanyika Uswisi na Ujerumani wamekwishatoa ratiba na inafahamika U20 ya TPM itacheza na timu gani.
    Michuano hiyo iliyopewa jina Blue Star Cup, mjini Zurich Jumatano ya Mei 16, saa 9:30 kwa saa za huko, Mazembe itacheza na wenyeji FC Blue Stars na siku hiyo hiyo saa 12:30 itacheza na Borussia Moenchengladbach.
    Alhamisi ya Mei 17, saa 3:15 asubuhi,  Mazembe itacheza na Grasshopper Club Zurich na saa 4:50 itacheza na Panathinaikos.
    Klabu sita Afrika zimepeleka timu zao za vijana kwenye michuano hiyo ya FIFA Blue Stars, ambazo na TPM, nyingine ni Al Ahly ya Cairo, Nania FC na Dwarfs za Ghana, Abuja Boys ya Nigeri na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
    Jumamosi ya Mei 26, saa 8:45 litafanyika gwaride rasmi la utambulisho wa timu katika ufunguzi wa michuano hiyo.
    Saa 10.50: Mazembe itacheza na FSV Mainz 05, Jumapili ya Mei 27, saa 12:45, Mazembe itacheza na TUS Ergenzingen na saa 11:55  Mazembe itacheza na timu ya taifa ya U-19 ya Bulgaria wakati Mei 28, saa 4:00 fainali zitaanza.
    Kumbuka kwenye kikosi cha wakubwa cha Mazembe kuna wachezaji wawili wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TIMU LA KINA SAMATTA LAENDA MASHINDANONI ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top