![]() |
| Mancini kulia na Balotelli mazoezini City |
MSHAMBULIAJI Mario Balotelli anataka
kubaki Manchester City, licha ya kocha Roberto Mancini kusema nyota huyo mtata
atapigwa bei mwishoni mwa msimu.
Kadi nyekundu ya nne aliyopewa Balotelli
ndani ya misimu miwili kwenye klabu hiyo, imemkatisha tama Mancini juu ya
nidhamu ya mchezaji huyo, lakini waka wa Mtaliano huyo, Mino Raiola amesema
mteja wake anataka kubaki Eastlands.
"Huu si wakati wa kurudi Italia.
Mario lazima aendelee na kujifunza England. Hatujaomba uhamisho wa Mario,"
Raiola alisema alipozungumza na Sky Sport baada ya kuulizwa kama Balotelli atarejea
Inter Milan au kujiunga na AC Milan.
"Mancini amekanusha kwamba
hataki kufanya chochote tenana Mario. Alitarajia adhabu kali na hawezi kumtumia
tena msimu huu."
Kadi nyekundu ya mwisho ya Balotelli
alipewa mwoshoni mwa wiki iliyopita City ikilala 1-0 mbele ya Arsenal kupewa
kadi ya pili ya njano, akianza kumchezea vibaya Bacary Sagna na baadaye Alex
Song.
"Kulikuwa kuna wakati wa
jazba, lakini sasa hali imetulia (kwa Mancini)," alisema Raiola.



.png)
0 comments:
Post a Comment