• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    BALOTELLI AZIKANA INTER MILAN, AC MILAN, ASEMA ANATAKA KUBAKI MAN CITY

    Mancini kulia na Balotelli mazoezini City
    MSHAMBULIAJI Mario Balotelli anataka kubaki Manchester City, licha ya kocha Roberto Mancini kusema nyota huyo mtata atapigwa bei mwishoni mwa msimu.
    Kadi nyekundu ya nne aliyopewa Balotelli ndani ya misimu miwili kwenye klabu hiyo, imemkatisha tama Mancini juu ya nidhamu ya mchezaji huyo, lakini waka wa Mtaliano huyo, Mino Raiola amesema mteja wake anataka kubaki Eastlands.
    "Huu si wakati wa kurudi Italia. Mario lazima aendelee na kujifunza England. Hatujaomba uhamisho wa Mario," Raiola alisema alipozungumza na Sky Sport baada ya kuulizwa kama Balotelli atarejea Inter Milan au kujiunga na AC Milan.
    "Mancini amekanusha kwamba hataki kufanya chochote tenana Mario. Alitarajia adhabu kali na hawezi kumtumia tena msimu huu."
    Kadi nyekundu ya mwisho ya Balotelli alipewa mwoshoni mwa wiki iliyopita City ikilala 1-0 mbele ya Arsenal kupewa kadi ya pili ya njano, akianza kumchezea vibaya Bacary Sagna na baadaye Alex Song.
    "Kulikuwa kuna wakati wa jazba, lakini sasa hali imetulia (kwa Mancini)," alisema Raiola.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BALOTELLI AZIKANA INTER MILAN, AC MILAN, ASEMA ANATAKA KUBAKI MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top