• HABARI MPYA

    Thursday, April 12, 2012

    MAN UNITED YATENGEWA TUZO KIBAO

    Uwanja wa Old Trafford unaotarajiwa kuipa tuzo Man United FC
    KLABU ya Manchester United imeingizwa kwenye kinyang’amyiro cha tuzo nne kutokana na kuboresha, bidhaa na maendeleo kwa ujumla na kupanua soko lake.
    Tuzo tatu za awali ni Tuzo za Biashara ya Uwanja, ambazo zitafanyika mjini Turin, Italia, Mei 15. Tuzo hizo zilianzishwa mwaka 2010, zinahusu mafanikio, ukarabati na fikra safi zinazoendana na dunia ya viwanja, utawala na uboreshaji wa maeneo ya michezo.
    Manchester United imeingizwa kuwania tuzo ya Mradi Bora wa Mwaka kwa kuendeleza eneo la jukwaa la vyumba la West Stand.
    Ubora wa mradi huo kwamba ni wa kisasa mno na umefanywa kuwa na vifaa ambavyo vinawawezesha mashabiki kujisikia raha wawapo eneo hilo na kuanzisha pia jukwaa lingine la maraha kwa ajili ya ‘watu wazito’ lenye mazingira ya kuvutia ile mbaya.
    Klabu hiyo pia imetajwa katika kuwania tuzo ya Ubora wa uhakika, ambayo inahusu mafanikio kwa ujumla, mafanikio ya uongozi katika matukio mbalimbali.
    Manchester United inatumai kukomba tuzo zote hizo tatu na kuwa klabu ya kwanza  Uingereza, Uwanja wake kumiliki heshima zote kubwa hizo tatu.
    Gwiji wa Manchester United, Gary Neville, ambaye hivi karibuni alipewa heshima ya Balozi wa Mazingira wa klabu, alisema: “Ni babu kubwa kuona Manchester United imepata heshima hii katika utawala wa mazingira. Nafahamu klabu ina jukumu kubwa la kuboresha zaidi mambo,”alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YATENGEWA TUZO KIBAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top