BAO LA YANGA LILIVYOPATIKANA NA ALIYEFUNGA HADI MTOA PASI
Winga wa Yanga, Simon Msuva akipiga kichwa kuelekeza langoni mwa MO Bejaia baada ya krosi ya beki wa kulia, Juma Abdul (hayupo pichani) katika mchezo wa Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 1-0
Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe akiunganisha mpira wa Msuva kuifungia Yanga bao pekee la ushindi kwenye mchezo huo
Tambwe alifanikiwa kuwazidi mabeki watatu na kipa wa MO Bejaia na kuutunbukiza mpira nyavuni
Pamoja na mpira kuvuka mstari, lakini mchezaji mmoja wa MO Bejaia aliurudisha uwanjani
Tambwe alipambana sana kwenye lango la MO Bejaia
Na baada ya kujiridhisha amefunga, akageuka kwenda kushangilia bao lake
Mabeki wa MO Bejaia walitaka kumdanganya refa, lakini hawakufanikiwa na bao hilo lilikubaliwa
Hapa Tambwe ananyoosha mkono kumpinga mshika kibendera aliyekataa bao hilo, lakii refa alikubali bao na Yanga imeshinda 1-0
0 comments:
Post a Comment