• HABARI MPYA

    Saturday, June 07, 2014

    KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2014; KUNDI B KUNA TIMU ZILIZOKUTANA FAINALI 2010, CHILE WASINDIKIZAJI?

    MABINGWA watetezi wa Kombe la Dunia, Hispania wapo kundi moja na Chile, Australia na washindi wa pili wa mwaka 2010, Uholanzi.
    BIN ZUBEIRY  inaendelea kukuketea makala za mchambuzi na beki wa zamani wa England, Martin Keown hapa akilichamua Kundi B.

    Hawafungiki kwa urahisi: Hispania insignia Brazil ikitoka kutwaa mataji matatu makubwa 
    Kundi B
    Hispania
    Uholanzi
    Chile
    Australia
    Utabiri wa Keown;
    1 Uholanzi
    2 Hispania
    3 Chile
    4 Australia
    Ratiba (Saa za Afrika Mashariki)
    Jun 13        Hipania v Uholanzi  Saa 4:00 usiku  Salvador
    Jun 13        
    Chile v Australia      Saa 7:00 usiku Cuiaba
    Jun 18        
    Australia v Uholanzi Saa 1:00 usiku P. Alegre
    Jun 18        
    Hispania v Chile       Saa 4:00 usiku R. Janeiro
    Jun 23        
    Australia v Hispania Saa 1:00 usiku  Curitiba
    Jun 23        
    Uholanzi v Chile       Saa 1:00 usiku Sao Paulo
    HISPANIA   
    Viwango vya FIFA: Namba 1
    Kocha: Vicente del Bosque. Kutwaa mfululizo Kombe la Dunia yatakuwa mafanikio makubwa.
    Nahodha: Iker Casillas (Real Madrid) 
    Mchezaji wa kumulikwa: Sergio Ramos (Real Madrid). Staili ya uchezaji ya viungo wa Hispania imekuwa kivutio, lakini mwishoni mea msimu Ramos alikuwa babu kubwa. Anaweza kumkabili mshambuliaji peyote na usomaji wake wa mchezaji umemfanya we bora na bora.
    Here they go again: Spanish defender Sergio Ramos got his hands on the World Cup four years ago
    Wanakwenda tena: Beki wa Hispaia, Sergio Ramos akiwaq ameinua Kombe la Dunia miaka mine iliyopita

    Ubora wao: Kukaa na mpira, hakuna ubishi kwamba linapokuja suala la kumiliki mpira, Hispania wanatisha- wanakaa na mpira 'siku nzima. 
    Hatari: Mabao yamepungua. Mwaka uliopita wameweza kufunga zaidi ya mabao mawili katika mechi mbili tu.
    Watakwenda England? Diego Costa yuko njiani kutua Chelsea wakati Cesc Fabregas anaweza kuungana naye earajani.
    Matokeo mazuri Kombe la dunia: Washindi (2010)
    Walivyofika hapa: Waliongoza kundi lao kwa rekodi ya kutopoteza mechi kati ya nane walizocheza, wakishinda sita na kutoa sare mbili.
    Je, wajua?: Mara ya mwisho nyavu za Hispania kuguswa katika hatua ya mtoano kwenye mashindano makubwa ilikuwa kwenye 16 bora ya Kombe la Dunia mwaka 2006.
    UHOLANZI
    Viwango vya FIFA: Namba 15
    Kocha: Louis van Gaal. Anakabiliwa na mtihani wa kuiongoza Uholanzi, wakati huo huo kufikiria namna ya kuisuka upya Man United.
    Nahodha: Robin van Persie (Manchester United)
    Dutch courage: Robin van Persie will be hoping Holland can go one better than four years ago
    Tegemeo la Uholanzi: Robin van Persie ana matumaini Uholanzi itafanya vizuri mwaka huu Kombe la Dunia zaidi ya miaka minne iliyopita

    Mchezaji wa kumulikwa: Daley Blind (Ajax). Mtoto wa shujaa wa zamani wa Uholanzi, Danny, ni mtaalamu haswa. Ameisaidia Ajax kushinda Ligi Kuu, akihamishwa kutoka kucheza beki ya kushoto hadi kiungo. 
    Ubora wao: Kutumia nafasi. Uholanzi imefunga mabao 34 katika mechi zao 10 za kufuzu.
    Hatari: Kumalizia mashindano. Uholanzi walifungwa kwa mara ya tatu wakifika fainali Kombe la Dunia mwaka  2010, rekodi ambayo sasa wanaishikilia wao na Ujerumani.
    Watakwenda England? Daley Blind, Daryl Janmaat, Bruno Martins Indi wametajwa Manchester United, Everton na Arsenal; Swansea wanampenda Jordy Clasie wakati Memphis Depay anavutiwa pia.
    Matokeo mazuri Kombe la Dunia: Washindi wa pili (1974, 1978 na 2010)
    Walivyofika hapa: Waliongoza kibabe kundi lao wakishinda mechi tisa kati ya 10 walizocheza. 
    Je, wajua? Hii ni mara ya pili Van Gaal anaiongoza timu hiyo ya taifa. Mara ya kwanza haikufuzu Kombe la Dunbia 2002 alipokuwa nayo.
    CHILE
    Viwango vya FIFA: Namba 14
    Kocha: Jorge Sampaoli. Muargentian aliyevuka mpaka hadi kutua Chile, anayetarajiwa kutamba na staili yake ya uvaaji kofia ya baseball.
    Nahodha: Claudio Bravo (Real Sociedad)
    Mchezaji wa kumulikwa: Alexis Sanchez (FC Barcelona). Ni mtu hatari kweli, ambaye alikuwa sababu ya England kufungwa na Chile Novemba mwaka jana. Anacheza pembeni ya Lionel Messi kwa Barcelona, lakini ni tegemeo kubwa la Chile katika safu ya ushambuliaji.
    Familiar face: Spain players will know all about Chile's Barcelona forward Alexis Sanchez
    Sura maarufu: Wachezaji wa Hispania wanamjua vizuri mshambuliaji wa Chile anayechezea Barcelona, Alexis Sanchez

    Ubora wao: Wanacheza kwa kasi na kujituma. Sampaoli anatumia mfumo sawa na wa Marcelo Bielsa aliyeiongoza timu hiyo mwaka 2010 wakati walipokuwa moja ya timu zilizoburudisha kwa soka maridadi kwenye michuano hiyo.
    Hatari: Kukosa Mwendelezo. Walishinda mechi tisa za kufuzu, sawa na Argentina, lakini wakafungwa sita, mbili na Argentina.
    Watakwenda England? Gary Medel ataondoka Cardiff lakini anaweza kurudi Hispania, Hull inampenda Jean Beausejour wakati United, Liverpool na Arsenal wote wanaweza kumtaka Sanchez iwapo dau watalimudu.
    Matokeo mazuri Kombe la Dunia: Mshindi wa 3 (1962)
    Walivyofika hapa: Walimaliza nafasi ya tatu kwenye kundi nyuma ya Argentina na Colombia, wakishinda mechi tisa kati ya 16, na kutoa sare moja tu.
    Je, wajua? Chile haijawahi kufika Fainali ya Kombe la Dunia, lakini walishika nafasi ya tatu katika Kombe la Dunia la U20 na U17 sambamba na Michezo ya Olimpiki
    AUSTRALIA
    Viwango vya FIFA: Namba 62
    Kocha: Ange Postecoglou. Muaustralian mzaliwa wa Ugiriki ana uzoefu na Kombe la Dunia– akiwa amewahi kuziongoza timu za vijana za U17 na U20 kwenye michuano hiyo ya FIFA.
    Nahodha: Mile Jedinak (Crystal Palace).
    Mchezaji wa kumulikwa: Matthew Ryan (FC Bruges). Kustaafu kwa Mark Schwarzer ni pigo kwenye lango la Australia, lakini mzuia michomo huyo kinda anaweza kuwa mrithi wake wa kudumu.
    Ubora wao: Mashambulizi yao ya nguvu ya krosi kutoka pembezoni mwa Uwanja yanatisha  huku Tim Cahill akitegemewa kumalizia.
    Hatari: Safu ya ulinzi shaka tupu. Kustaafu kwa wachezaji wake wazoefu kumepunguza uimara wa safu ya ulinzi ya Australia. 
    Watakwenda England? Hakuna mengi ya kuandika juu ya Jedinak, lakini Tommy Oar mwenye umri wa miaka 22, wing anayechezea FC Utrecht nchini Uholanzi ndiye pekee ambaye klabu zinamfuatilia.
    Matokeo mazuri Kombe la Dunia: 16 Bora (2006)
    Walivyofika hapa: Walishika nafasi ya pili katika kundi la Asia kufuzu Kombe la Dunia, wakizidiwa pointi nne na vinara Japan.  
    Je, wajua? Tim Cahill hive karibuni alipewa heshima ya kipekee baada ya barabara mjini Sydney kupewa jina lake ‘Tim Cahill Expressway’.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2014; KUNDI B KUNA TIMU ZILIZOKUTANA FAINALI 2010, CHILE WASINDIKIZAJI? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top