BEKI David Luiz amekamilisha uhamisho wake kutoka Chelsea kutua Paris St Germain kwa kusaini Mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa Ufaransa.
Luiz - ambaye aliichezea Selecao jana katika mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia ikishinda 3-1 dhidi ya Croatia anaondoka Stamford Bridge kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 50, hivyo anakuwa beki ghali zaidi duniani.
Klabu hiyo ya Ufaransa imetangaza katika tovuti yake kwamba; "Paris Saint-Germain inayo furaha kutangaza kukamilisha usajii wa mwanasoka wa kimataifa wa Brazil, David Luiz kutoka Chelsea FC, atakayekuwa wetu kwa miaka mitano ijayo,".

Shangwe za ushindi wa jana: David Luiz akishangilia ushindi wa jana wa Brazil. Beki huyo amesaini mkataba wa miaka mitano PSG


.png)
0 comments:
Post a Comment