• HABARI MPYA

    Wednesday, September 25, 2013

    NEYMAR, MESSI WAFUNGA WOTE BARCA IKIUA 4-1 LA LIGA

    IMEWEKWA SEPTEMBA 25, 2013 SAA 12:31 ASUBUHI
    WACHEZAJI nyota duniani, Neymar na Lionel Messi wote walifunga mabao jana kwa mara ya kwanza wakati Barcelona inaendeleza wimbi lake la ushindi La Liga kufuatia ushindi wa 4-1 dhidi ya Real Sociedad Uwanja wa Nou Camp.
    Barcelona imeendeleza rekodi nzuri katika harakati za kutetea taji, huku Neymar akifunga bao lake la kwanza La Liga na Messi akifunga bao lake la saba msimu huu.
    Neymar alifungua karamu ya mabao ya Barca dakika ya tano, kabla ya Messi kufunga la pili dakika tatu baadaye, Busquets la tatu dakika ya 23 na Bartra kuhitimisha dakika ya 77.
    Bao pekee la kufutia machozi la wageni lilifungwa na De la Bella dakika ya 64.
    Kikosi cha Barcelona jana kilikuwa: Valdes; Alves, Pique, Mascherano, Adriano; Busquets, Xavi, Iniesta; Sanchez, Messi na Neymar.
    Real SociedadBravo; Estrada, Cadamuro, Martinez, De la Bella; Bergara, Ros, Prieto, Sangalli; Seferovic, Griezmann.
    Lionel Messi
    Wawili, mawili: Lionel Messi akishangilia bao lake alilotengenezewa nafasi ya kufunga na Mbrazil, Neymar 
    Neymar
    La kwanza kati ya mengi: Neymar akipiga ngumi hewani kushangilia bao lake la kwanzkufunga La Liga
    Neymar
    Kijana kutoka Brazil: Neymar akipongezwa na wachezaji wenzake 
    BARCELONA
    Neymar
    Hisi upendo: Neymar na Messi wakionyesha watoto wao kabla ya mechi na kulia wakipongezana baada ya mechi
    Sergio Busquets
    Mtu mrefu: Sergio Busquets (katikat) akiwapa tano wenzake baada ya kufunga
     Lionel Messi
    Mashine: Lionel Messi akijaribu kupasua ukuta wa Sociedad 
    Marc Bartra
    Bao la mwisho: Beki wa Barca, Marc Bartra (wa pili kushoto) alihitimisha karamu ya mabao ya Barca kwa bao la nne
    Barcelona
    Mchuano: Sergio Busquets (kushoto) akigombea mpira na mshambuliaji wa Real Sociedad, Imanol Agirretxe
    Barcelona
    Kazi kazi: Andres Iniesta (kulia) akipambana na Inigo Martinez Berridi
    Barcelona
    Gerard Pique (kushoto) akimtoka kiungo wa Sociedad, Markel Bergara Larranaga 
    Alexis Sanchez
    Alexis Sanchez wa Barca akigombea mpira na Alberto de la Bella
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NEYMAR, MESSI WAFUNGA WOTE BARCA IKIUA 4-1 LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top