• HABARI MPYA

    Sunday, September 29, 2013

    MANCINI ATUA UTURUKI KUSAINI MKATABA MNONO WA KUIFUNDISHA GALATASARAY

    IMEWEKWA SEPTEMBA 29, 2013 SAA 2:08 USIKU
    KOCHA Roberto Mancini leo amekwenda mjini Istanbul, Uturukikufanya mazungumzo ya kusaini Mkataba wa miaka mitatu kuifundisha Galatasaray utakaokuwa na thamani ya Pauni Milioni 4.6 kwa mwaka.
    Mancini, amekuwa 'juu ya mawe' tangu atupiwe virago Manchester City mwishoni mwa msimu na anatarajiwa kutambulishwa kurithi mikoba ya Fatih Terim Jumanne.
    Mabingwa hao wa Uturuki pia wamekubali kumlipa Mtaliano huyo bonasi ya Pauni Milioni 5.86 kama watavuka hatua waliyofika mwaka jana Ligi ya Mabingwa na kufanikiwa kuingia Robo Fainali.
    Sorted: Roberto Mancini is in Turkey completing negotiations over a three-year deal at Galatasary
    Kimeeleweka: Roberto Mancini yupo Uturuki kukamilisha mazungumzo ya kujiunga na Galatasary
    Not out of work for long: Mancini was sacked by Manchester City in May
    Juu ya mawe noma: Mancini alifukuzwa Manchester City Mei, mwaka huu
    Mancini anatarajiwa kukutana na Rais wa klabu, Unal Aysal Jumatatu kufikia makubaliano ya mwisho ya Mkataba, kwa mujibu wa wakala Muzzi Ozcan ambaye alifanikisha kuziunganisha pande hizo mbili, baada ya klabu hiyo kumfukuza Terim.
    Coup: Galatasaray's move for the Italian is a big statement of intent
    Uturuki sasa: Galatasaray inamtaka Mtaliano huyu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MANCINI ATUA UTURUKI KUSAINI MKATABA MNONO WA KUIFUNDISHA GALATASARAY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top