• HABARI MPYA

    Thursday, September 26, 2013

    MAN UNITED YAICHAPA LIVERPOOL 1-0 KOMBE LA LIGI

    IMEWEKWA SEPTEMBA 26, 2013 SAA 6:01 USIKU
    MACHO yote yalikuwa kwa Luis Suarez baada ya kurejea Liverpool kufuatia kumaliza adhabu yake ya mechi 10, lakini Javier Hernandez akaiteka shoo kwa bao lake pekee lililoipeleka Manchester United Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One.
    Hatimaye Suarez alicheza mechi yake ya kwanza ya msimu mpya baada ya kumaliza kutumikia adhabu yake ya kumng'ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic msimu uliopita.
    Na wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay alizomewa na mashabiki Uwanja wa Old Trafford, alikuwa ni Chicharito aliyepoza maumivu ya David Moyes kufuatia kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa wapinzani, Manchester City katika Ligi Kuu Jumapili.
    Liverpool ilitawa sehemu kubwa ya mchezo na Daniel Sturridge alipoteza nafasi kadhaa nzu za kufunga, lakini Hernandez hakufanya makosa alipopata nafasi dakika ya 46.
    Wayne Rooney, ambaye ndiye mchezaji bora zaidi kwa United hivi sasa, alipiga kona nzuri baada ya mapumziko na Hernandez akaunganisha nyavuni.
    Kikosi cha Manchester United kilikuwa: De Gea, Rafael Da Silva, Smalling, Evans, Buttner, Jones, Giggs, Nani, Rooney, Kagawa na Hernandez. 
    Liverpool: Mignolet, Toure, Skrtel, Sakho, Jose Enrique, Gerrard, Lucas, Henderson, Suarez na Moses, Sturridge.  
    Roar: Javier Hernandez celebrates after handing Manchester United the lead at Old Trafford
    Shujaa: Javier Hernandez akishangilia baada ya kufunga bao pekee la Manchester United Uwanja wa Old TraffordCheck the technique: Hernandez leaps into the air as Wayne Rooney's corner found him free in the penalty area
    Angalia maujuzi: Hernandez akienda hewani kuunganisha kona ya Wayne Rooney... Hernandez contorts his body to flick the ball on the volley into the Liverpool net while in mid-air
    ... Hernandez alivyofungaThat's better: David Moyes celebrates Hernandez's goal after the misery of Sunday's derby defeat
    Hiyo babu kubwa: David Moyes akishangilia bao la HernandezLook who's back: Luis Suarez looked happy to be in the Liverpool side again as he warmed up for the match
    Amerudi: Luis Suarez akionekana mwenye furaha kuwa kikosini Liverpool tenaExchanging pleasantries: Suarez shakes hands with Wayne Rooney before the match
    Suarez akipeana mikono na Wayne Rooney kabla ya mechiSaved: The Uruguay striker nearly got in on goal in the first half but was shut out by United keeper David De Gea
    Suarez alikaribia kufunga kipindi cha kwanza, lakini kipa wa United, David De Gea akaokoaIn the action: Suarez gets a header in as United left back Alex Buttner watches on
    Suarez akipiga kichwa huku beki wa kushoto wa United, Alex Buttner akimuangaliaOuch: United defender Phil Jones fouls Suarez with a crunching tackle
    Yalaa: Beki wa United, Phil Jones akimchezea rafu SuarezNot enjoying the match, Roy? United legend Keane was in the stands watching the action
    Gwiji wa United, Roy Keane alikuwa jukwaani akiangalia mechiFull blooded: Rooney shows his commitment in the tackle with Mamadou Sakho
    Rooney akipambana na Mamadou Sakho
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAN UNITED YAICHAPA LIVERPOOL 1-0 KOMBE LA LIGI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top