IMEWEKWA SEPTEMBA 2, 2013 SAA 2:14 USIKU
KLABU ya Liverpool imethibitisha kusajili mabeki Tiago Ilori kutoka Sporting Lisbon na Mamadou Sakho kutoka Paris Saint-Germain.
Wachezaji wote hao waliishuhudia timu hiyo jana ikiilaza 1-0 Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England katika jukwaa la madakatri Uwanja wa Anfield na walisaini mikataba yao baada ya kukamilisha vipimo vya afya katika Uwanja wa mazoezi wa klabu, Melwood.
Ilori, aliyezaliwa London, amezichezea timu za taifa za vijana za Ureno chini ya umri wa miaka 18, 19 na 20.
Silaha mpya: Ilori ni mchezaji wa sita kusajiliwa Liverpool majira haya ya joto
Sakho akionyesha jezi yake mpya
Ilori (katikati) akiwa na Sakho (kushoto) na mchezaji mwingine mpya, Victor Moses (kulia) Uwanja wa Anfield jana


.png)