Mashabiki wa Azam wakiishangilia timu yao leo Chamazi |
Kiungo wa Azam FC, Jabir Aziz Stima akipasua katikati ya wachezaji wa African Lyon |
Urithi wa Baba; Mtoto Raiyan akiwa amebebwa na baba yake, Salum Nassor wote wamevaa jezi za Azam leo Chamazi. Kushoto ni rafiki yake Salum, Abdulhadi |
Joackins Atudo wa Azam FC akigombea mpira wa juu na mshambuliaji wa Lyon |
Ushindi raha; Kocha wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall akitembea kwa madaha Chamazi leo |
Mfungaji wa mabao mawili ya Azam FC leo, Kipre Tchetche akiwatoka mabeki wa Lyon |
Wamemkalisha; Kipre Tchetche akiwa chini baada ya kuangushwa na mabeki wa Lyon |
Chenga; Kiungo wa Azam FC, Humphrey Mieno aliyetoa pasi ya bao la tatu lililofungwa na Kipre Tchetche akimlamba chenga beki wa Lyon kabla ya kutoa pasi ya bao |
Mieno na Kipre wakishangilia matunda ya kazi yao |
Mieno akimuacha chini beki wa Lyon tayari kutoa pasi ya bao |
Furaha ya ushindi; Wachezaji wa Azam wakishangilia |
Ushindi raha bwana |
Wastaafu; Wachezaji wa zamani wa timu mbalimbali, kutoka kulia Habib Kondo, Ngawina Ngawika, Yahya Issa, Abubakar Mtiro na Victor Costa wakifuatilia mechi hiyo leo |