• HABARI MPYA

    Friday, April 19, 2013

    KLABU TAJIRI DUNIANI, MAN UNITED YAIACHIA USUKANI REAL MADRID, CHELSEA NA MAN CITY HAWAIPATI NG'O ARSENAL KWA MIHELA


    KLABU ya Manchester United ya England imeng'olewa kileleni katika orodha ya jarida la Forbes la klabu tajiri duniani na sasa vigogo wa Hispania, Real Madrid ndio wanaongoza.
    United imekuwa kileleni tangu wachambuzi wa biashara wa Forbes waanze kuorodhesha klabu tajiri duniani mwaka 2004, lakini sasa imepigwa bao na Real.
    Barcelona inashika nafasi ya tatu na Arsenal ni ya nne mbele ya Bayern Munich iliyo katika nafasi ya tano.
    Overtaken: Manchester United were knocked off the top spot in Forbes' football rich list
    Wamepitwa: Manchester United wameporomoka nafasi moja katika orodha ya klabu tajiri kwenye jarida la Forbes
    Top dogs: Spanish giants Real Madrid are valued at £2.15billion
    Wako juu: Vigogo wa Hispania, Real Madrid wana thamani ya Pauni Bilioni 2.15

    Real ina thamani ya Pauni Bilioni 2.15 (sawa na dola za Kimarekani Bilioni 3.3) - hivyo kuifanya klabu hiyo ya Hispania kuwa chombo cha michezo chenye thamani kubwa zaidi duniani- na United wana thamani ya Pauni Bilioni 2.07.
    Sneaking into the top four: Arsenal are fourth on the list behind Real Madrid, Manchester United and Barcelona
    Wamo nne bora: Arsenal wanashika nafasi ya nne nyuma ya Real Madrid, Manchester United na Barcelona

    10 BORA YA KLABU TAJIRI DUNIANI ZA FORBES...

    TOP 10 RICH LIST

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KLABU TAJIRI DUNIANI, MAN UNITED YAIACHIA USUKANI REAL MADRID, CHELSEA NA MAN CITY HAWAIPATI NG'O ARSENAL KWA MIHELA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top