• HABARI MPYA

    Sunday, April 21, 2013

    YANGA NA JKT RUVU ILIKUWA TAMU AJE LEO...HIVI NDIVYO WATOTO WA JANGWANI WALIVYOPELEKA POSA YA MWALI

    Beki wa JKT Ruvu, Stanley Nkomola akijaribu kumzuia mshambuliaji wa Yanga SC, Simon Msuva katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 3-0.

    Utamu wa bao; Nizar Khalfan akishangilia bao lake la tatu aliloifungia Yanga leo

    Kipa wa JKT Ruvu, Shaaban Dihile akidaka mpira wa juu

    Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima akifuarahia baada ya krosi yake kuzaa bao

    Mkamate kama unaweza; Msuva akiambaa na mpira dhidi ya Damas Makwaya wa JKT

    Mabingwa watarajiwa; Kikosi cha Yanga SC leo

    Kikosi cha JKT Ruvu leo

    Katikati ya dimba; Kiungo wa Yanga, Frank Domayo akimdhibiti kiungo wa JKT Ruvu mbele yake

    Yanga TV; Shabiki wa Yanga akiwa na kitu mfano wa kamera

    Hunitishi; Simon Msuva wa Yanga akizozana na Haroun Adolph wa JKT Ruvu

    Kombe bandia; Mashabiki wa Yanga wakishangilia na Kombe la 'kubumba'

    Kwa raha zao; Mashabiki wa Yanga, cheki huyo ambaye yuko na mtoto wake, anamuambukiza maradhi mapemaaa

    Anachungulia; Haruna Niyonzima akijiandaa kupiga krosi iliyozaa bao la tatu

    Busu motomoto; Nahodha wa Yanga, Nador Haroub 'Cannavaro' akimpiga busu Simon Msuva baada ya kufunga

    Simon Msuva akimpongeza Hamisi Kiiza kufunga bao la pili

    Amewanyonga; Msuva akiwakebehi mashabiki wa Simba waliokuwa wakiishangilia JKT Ruvu baada ya kufunga

    Mwanariadha?Msuva akikimbia kushangilia bao lake 

    Athumani Iddi 'Chuji' akimiliki mpira mbele ya kiungo wa JKT Ruvu,  Nashon Naftali, huku Haruna Niyonzima akiwa tayari kutoa msaada 

    David Luhende wa Yanga akimtoka Hassan Kikutwa wa JKT Ruvu

    Nizar Khalfan akichanja mbuga... 

    Hawa vipi? Kipa Shaaban Dihile nyuma akiwa amenagukiwa na beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' katika moja ya hekaheka za mechi hiyo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA NA JKT RUVU ILIKUWA TAMU AJE LEO...HIVI NDIVYO WATOTO WA JANGWANI WALIVYOPELEKA POSA YA MWALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top