• HABARI MPYA

    Tuesday, April 23, 2013

    VAN PERSIE APIGA ZOTE MAN UNITED IKIUA 3-0 NA KUTWAA RASMI UBINGWA WA LIGI KUU ENGLAND, MAN CITY DORO


    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uholanzi, Robin van Persie ameihakikishia ubingwa wa 20 wa Ligi Kuu ya England Manchester United usiku huu baada ya kufunga mabao yote katika ushindi wa 3-0 Uwanja wa Old Trafford dhidi ya  Aston Villa walio kwenye hatari ya kushuka.
    Van Persie alipiga Hat-trick hiyo ndani ya dakika 33 za mechi hiyo, likiwemo bao lililoingia kwenye kinyang'anyiro cha bao bora la msimu alipounganisha moja kwa moja pasi ndefu ya Wayne Rooney akiwa nje kidogo ya eneo la hatari.
    Mdachi huyo, aliyeamua kujiunga na kikosi cha Sir Alex Ferguson badala ya Manchester City ya Roberto Mancini msimu huu akitokea Arsenal, alifunga mabao yake katika dakika za pili, 12 na 33, mawili pasi za Rooney  na moja pasi ya Ryan Giggs.
    Ferguson leo alichezesha viungo watatu katikati, Shinji Kagawa, Michael Carrick na Rooney aliyekuwa akiichezesha timu mbili na kufanya kazi nzuri ya kupendeza, akitoa pasi mbili za mabao kabla ya kumpisha Danny Wellbeck dakika ya 72.
    Kikosi cha Man United leo kilikuwa; De Gea, Rafael, Evra,  Jones, Evans, ValenciaGiggs, CarrickKagawa, Rooney/Welbeck dk72 na Van Persie
    Aston Villa; Guzan, Vlaar, Bennett/Clark dk80,Baker, Lowton, N'Zogbia/El Ahmadi dk46,Westwood, Delph, Agbonlahor, Benteke na Weimann
    Relief: Robin van Persie holds his arms aloft after securing the title for Manchester United
    Ahueni: Robin van Persie akiinua mikono yake juu baada ya kuihakikishia ubingwa Manchester United
    Out with a bang: Robin van Persie's second goal was a joy to behold and set United on course
    Bao la msimu: Robin van Persie akifunga bao la pili
    Out with a bang: Robin van Persie's second goal was a joy to behold and set United on course
    Out with a bang: Robin van Persie's second goal was a joy to behold and set United on course
    One hand on the trophy: Van Persie celebrates scoring his hat-trick goal after 33 minutes
    Mkono mmoja kwenye taji: Van Persie akishangilia baada ya kukamilisha Hat-trick dakika ya 33Credit where it's due: Van Persie picks Wayne Rooney up after he picked the Dutchman out for his wonder goal
    Asante ya pasi ya bao: Van Persie akimuinua Wayne Rooney baada ya kumpa pasi ya bao zuri
    Early doors: Van Persie scored his first after just two minutes on the pitch
    Kitu: Van Persie akifunga bao la kwanzaGive us a wave: Ferguson knows he has one hand on the trophy with a few minutes to play
    Kwaheri Mancini: Ferguson akinyoosha mkono kwa ishara wa kuwaacha porini Man City katika mbio za ubingwa
    Get that changed: This banner will have to be replaced before the next game at Old Trafford
    Lahitaji marekebisho: Bango hili litatakiwa kubadilishwa kabla ya mechi ijayo Old Trafford
    Van Persie
    Van Persie
    Ni tofauti? Van Persie na United wamekuwa na msimu mzuriTussle: Nathan Baker appears to climb on the back of United's Shinji Kagawa when they vie for the ball
    Mchuano: Nathan Baker akimpanda Shinji Kagawa wakati wakigombea mpira
    .Hard work: Christian Benteke (right) had a big task playing up front on his own for Villa
    Kazi ngumu: Christian Benteke (kulia) akipambana na Patrice Evra
    Never in doubt: United fans hold up flags and scarves before the match against Aston Villa
    Hakuna shaka: Mashabiki wa United wakiwa na bendera  kabla ya mechi na Aston Villa
    Never in doubt: United fans hold up flags and scarves before the match against Aston Villa

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: VAN PERSIE APIGA ZOTE MAN UNITED IKIUA 3-0 NA KUTWAA RASMI UBINGWA WA LIGI KUU ENGLAND, MAN CITY DORO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top