• HABARI MPYA

    Tuesday, April 30, 2013

    RONALDO LIMA ATOA NUKSI MARACANA, AFUNGA BAO LAKE LA KWANZA JANA USIKU KATIKA SHEREHE ZA UFUNGUZI BAADA YA UKARABATI WA MIAKA MITATU


    UWANJA maarufu wa Brazil, Maracana Stadium umefunguliwa tena jana usiku baada ya miaka  mitatu ya ukarabati, na upo tayari kwa fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 na sherehe za ufunguzi za Olimpiki ya mwaka 2016.
    Mchezo wa kwanza kufanyika kwenye Uwanja huo baada ya kukamilika kwa ukarabati wake uliikutanihsa timu ya Marafiki wa wa Ronaldo dhidi ya Marafiki wa Bebeto jana.
    Rais wa Brazil, Dilma Rousseff, rais wa zamani, Luiz Inacio Lula da Silva na watu wengine wenye majina makubwa waliokuwa miongoni mwa watu 30,000 waliohudhuria ufunguzi huo.
    Washington, mshambuliaji wa zamani wa Fluminense, alifunga bao la kwanza jana kwa kichwa dakika ya 16, wakati Ronaldo, ambaye enzi zake anacheza hakuwa kufunga kabisa kwenye Uwanja huo, jana alifunga bao lingine.
    Maracana ulikuwa mmoja wa viwanja vikubwa duniani, wakati watu 200,000 waliposhuhudia Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1950 kati ya Brazil na Uruguay. Pia ni uwanja ambao, Pele alifunga bao lake la 1,000 mwaka1969.

    'Temple of Football': The renovated Maracana Stadium in Rio de Janeiro, Brazil re-opened last night as two teams of Brazilian legends, led by Ronaldo and Bebeto, played each other
    'Sinagogi la Soka': Ukarabati umekamilika Uwanja wa Maracana uliopo Rio de Janeiro, Brazil na umefunguliwa jana kwa magwiji wa soka Brazil, wakiongozwa na Ronaldo na Bebeto kucheza baina yao.
    Honour: Welder Antonio Pereira joined Brazil legend Ronaldo in a ceremonial kick-off in front of a 30,000 crowd made up largely of the stadium's construction workers and their families
    Heshima: Welder Antonio Pereira aliungana na gwiji wa Brazil, Ronaldo katika sherehe za ufunguzi
    First of many: The former Brazilian international Washington had the distinction of scoring the first goal at the 'new' Maracana after three years of upgrades in time for next summer's World Cup and the 2016 Olympics
    Bao la kwanza: Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Washington alifunga bao la kwanza jana katika Maracana mpya
    Hallowed turf: Washington kisses the pitch after scoring the opener
    Busu la uepndo: Washington akibusu nyasi za Uwanja  huoProtest: A few hundred people held a peaceful demonstration against the privatisation of the stadium development, claiming the government will lose money on their investment
    Mamia kadhaa walikandia zoezi hilo kwa njia ya amani, wakibeba mabango ya kubeza kwamba Serikali ya nchi hiyo itapata hasara katika uwekezaji wake huo
    Storm: Police forcibly arrest a protestor outside the Maracana during demonstrations against the privatisation of the stadium on Friday
    Timbwili: Polisi wakiwakamata watu waliokuwa wakifanya vurugu nje ya Uwanja wa Maracana Ijumaa
    Scuffle: A female demonstrator is detained by armed police during Friday's protests
    Welder Antonio Pereira alipewa heshima ya kwenda kumpasia mpira Ronaldo kuanzisha mchezo huo wa sherehe za ufunguzi.
    Ronaldo, ambaye aliiwezesha Brazil kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1994 na 2002, pia ni Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Fainali zijazo za Kombe la Dunia
    Legend: Two-time World Cup winner Ronaldo waves to the crowd. Incredibly, he did not score at the Maracana during his professional career
    Gwiji: Mshindi wa fainali mbili za Kombe la Dunia, Ronaldo akiupungia umati jana. Enzi zake anacheza soka hakuwaghi kufunga bao Uwanja wa Maracana
    Still got it: Ronaldo, who scored 62 goals in 98 matches for Brazil, picks a pass during the test match
    Bado anaweza: Ronaldo, aliyeifungia Brazil mabao 62 katika mechi 98, akipokea pasi jana
    Pace: Ronaldo skips past Roger during the exhibition match
    Anakumbushia: Ronaldo akipasua...
    Veteran: Bebeto, who was captain of the other team, takes on a player during the match
    Mkongwe: Bebeto, ambaye alikuwa  Nahodha wa timu nyingine, akimtoka mchezaji jana
    On the ball: The Brazil veteran Junior, who won 70 caps, takes play forward
    Anakwenda na mpira: Mkongwe wa Brazil, Junior, ambaye aliichezea Brazil mechi 70, akiambaa na mpira jana

    VIDEO: Ronaldo akifunga Maracana

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: RONALDO LIMA ATOA NUKSI MARACANA, AFUNGA BAO LAKE LA KWANZA JANA USIKU KATIKA SHEREHE ZA UFUNGUZI BAADA YA UKARABATI WA MIAKA MITATU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top