• HABARI MPYA

    Friday, April 26, 2013

    CHELSEA WAIKUNG'UTA 2-1 BASLE BARAZANI KWAKE....SASA WANUSA FAINALI ULAYA

    Last gasp: David Luiz struck with what proved to be the final kick of the game

    Bao dakika ya mwisho: David Luiz akifunga kwa mpira wa adhabu kuipa ushindi wa 2-1 Chelsea ugenini usiku huu
    Pure delight: Luiz celebrates wildly after scoring with a low free-kick
    Shangwe zake: Luiz akishangilia baada ya kufunga
    Tucked away: Fabian Schar converted after a penalty was awarded for very little at all
    Penalti ya utata: Fabian Schar akiifungia Basle kwa penalti bao la kusawazisha  


    BAO la dakika ya mwisho la mpira wa adhabu uliotinga moja kwa moja nyavuni la David Luiz limeipa ushindi wa mabao 2-1 Chelsea katika Nusu Fainali ya kwanza ya Europa League ugenini dhidi ya wenyeji Basle. 
    Awali, alinusurika kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kudaiwa kucheza rafu.
    Refa Pavel Kralovec alitoa uamuzi wa ajabu sana alipodai Luiz kamchezea rafu Cesar Azpilicueta kwenye eneo wakati hakucheza na akawapa penalti wenyeji wakapata bao la kusawazisha lililofungwa na Fabian Schar dakika ya 87.
    Chelsea ilikuwa ya kwanza kupata bao lililofungwa na Victor Moses dakika ya 12.
    Kikosi cha Basle kilikuwa: Sommer, Philipp Degen, Schar, Dragovic, Park, Fabian Frei, Salah/Degan dk78, El-Nenny/Zoua dk65, Die/Diaz dk61, Stocker na Streller. 
    Chelsea: Cech, Azpilicueta, Ivanovic, Terry, Cole, Luiz, Hazard/Mata dk71, Ramires, Lampard/Oscar dk79, Moses na Torres. 
    Katika Nusu Fainali nyingine, Fenerbace imeilaza 1-0 nyumbani Benfica, bao pekee la Korkmaz dakika ya 72.
    Away goal: Victor Moses' (right) header opened the scoring for Chelsea
    Bao la kwanza: Victor Moses (kulia) akiifungia Chelsea
    Topsy-turvy: The Nigerian winger celebrated in style
    Topsy-turvy: The Nigerian winger celebrated in style
    Sarakasi za shangwe: Winga Mnigeria akishangilia kwa sarakasi za aina yake
    Aiming high: Rafa Benitez wants to take Chelsea to Europa League glory this season
    Malengo makubwa: Rafa Benitez anataka kuipa Chelsea taji la Europa League msimu huu
    Magic man: Until he was substituted, Eden Hazard was the star of the show
    Mchawi: Hadi anatolewa, Eden Hazard alikuwa nyota wa mchezo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: CHELSEA WAIKUNG'UTA 2-1 BASLE BARAZANI KWAKE....SASA WANUSA FAINALI ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top