• HABARI MPYA

    Tuesday, April 23, 2013

    BARTHEZ WA YANGA AITWA STARS MPYA YA KUSUBIRI

    Ally Mustafa 'Barthez'

    Na Boniface Wambura
    KIPA wa Yanga SC, Ally Mustafa ‘Barthez’ amejumuishwa katika kikosi cha wachezaji 30 wa timu ya pili ya taifa, Young Taifa Stars kilichotajwa leo na kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mdenmark, Kim Poulsen.
    Poulsen amesema ataitumia timu hiyo B ya taifa, kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya kwanza, A.
    Akizungumza na Waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (Aprili 23 mwaka huu) kabla ya kutaja kikosi hicho, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.
    Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini atatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.
    “Timu hii ni kiungo kati ya vijana na wakubwa. Wengi wa wachezaji watakuwa vijana, lakini wakubwa wachache watapata fursa ya kuwemo ili kuangalia uwezo wao hata kama uko nyuma waliwahi kuchezea Taifa Stars. Lakini timu hii vilevile ni changamoto wa wachezaji wa Taifa Stars kuwa wapo wanaosubiri wazembee ili wachukue nafasi zao,” amesema.
    Young Taifa Stars yenye wachezaji 30 itakuwa na kambi ya siku tano jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 2 hadi 6 mwaka huu.
    Wachezaji walioitwa ni Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Ali Mustapha ‘Barthez’ (Yanga) ambao ni makipa. Mabeki ni Kessy Hassan (Mtibwa Sugar), Kennan Ngoma (Barnsley FC, Uingereza), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), David Mwantika (Azam), Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Kagera Sugar), Waziri Salum (Azam), Samih Nuhu (Azam) na Emily Mgeta (Simba).
    Viungo ni Haruna Chanongo (Simba), Edward Christopher (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), William Lucian (Simba), Jonas Mkude (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Jimmy Shoji (JKT Ruvu), Abdallah Seseme (Simba), Ramadhan Singano (Simba), Farid Mussa (Azam) na Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar).
    Washambuliaji ni Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Jerome Lambele (Ashanti United), Zahoro Pazi (JKT Ruvu), Twaha Hussein (Coastal Union), Seif Abdallah Karihe (Azam) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BARTHEZ WA YANGA AITWA STARS MPYA YA KUSUBIRI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top