• HABARI MPYA

    Wednesday, October 17, 2012

    JOEY BARTON AMESHINDIKANA DUNIA NZIMA, AMTANDIKA MTU KIATU HICHO!


    KIUNGO Joey Barton ameshindikana na hawezekani popote! Tayari ameingia kwenye kashfa nyingine ya mchezo usio wa kiungwana akiwa katika klabu yake mpya, Marseille.
    Kiungo huyo alijiunga na timu hiyo ya Ufaransa Agosti baada ya kufungiwa mechi 12 akiwa anachezea Queens Park Rangers msimu uliopita.
    Lakini inaonekana Barton ameshindwa kubadilika kitabia hata baada ya kuhamia timu ya Ligue 1, baada ya kumchapa kiatu mchezaji wa Istre, Guy-Roland Niangbo.
    Aggressive: Joey Barton tackles FC Istres's Guy-Roland Niangbo during a friendly
    Cheki Joey Barton anavyomtandika kiatu mchezaji wa FC Istres, Guy-Roland Niangbo katika mechi ya kirafiki
    Separated: Barton and Niangbo square up after the tackle
    Hapa wanatenganishwa Barton na Niangbo baada ya kutaka kugombana

    Hii inaweza kumuweka pabaya Barton anayejaribu kutafuta fitness ya kucheza mechi kabla ya kuanza kuichezea klabu hiyo kwenye ligi.
    Lakini tukio hilo linakuja siku kadhaa baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 kukwaruzana na kipa wa AEL Limassol, Matias Degra katika Ligi ya Mabingwa.
    Pia Barton haruhusiwi kucheza Ulaya, hadi Novemba 17 wakati Marseille itakapomenyana na Bordeaux.
    Muingereza huyo alikiri hivi karibuni kwamba kadi nyekundu aliyopewa katika mechi ya mwisho ya Ligi Kuu England dhidi ya Manchester City, Mei mwaka huu ilimuangusha sana.
    Crash: Barton is unnecessarily late on Niangbo during the friendly (above) but still pointed the finger (below)
    Barton anampa mtu kitu hapo..hebu cheki....
    Crash: Barton is unnecessarily late on Niangbo during the friendly (above) but still pointed the finger (below)

    Barton aligombana na Carlos Tevez akapewa kadi nyekundu baada ya kugombana na wachezaji wengine wa City, Sergio Aguero na Vincent Kompany kabla ya kumvaa Mario Balotelli.

    SOURCE: http://www.dailymail.co.uk
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: JOEY BARTON AMESHINDIKANA DUNIA NZIMA, AMTANDIKA MTU KIATU HICHO! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top