• HABARI MPYA

    Saturday, October 27, 2012

    AZAM AKADEMI WAICHAPA SIMBA B

    Azam B imeifunga Simba B 1-0, bao pekee la Kevin Friday dakika ya 56 katika mchezo wa utangulizi kabla ya mechi za timu za wakubwa za klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.  Pichani wachezaji wa Azam B, maarufu kama Azam Academy wakishangilia bao lao pekee la ushindi kwa kumpongeza mfungaji, Kevin kulia. Tazama picha zaidi za mechi hiyo.

    Kocha wa makipa wa Simba, James Kisaka akishuhudia mechi hiyo

    Makocha Waserbia, Boris Bunjak wa Azam kushoto na Milovan Cirkovick wa Simba kulia wakijadiliana huku wakiangalia mechi hiyo  

    Mgaya Abdul wa Azam akikokota mpira, dhidi ya Miraj Athumani wa Simba. Kulia ni Abdallah Seseme aliyeipa mgongo kamera

    Mgaya Abdul akipiga mpira mbele ya Omary wa Simba

    Jamil Mchauro wa Azam akitoa pasi kwa Mange Chagula mbele ya Kemmy Ally wa Simba

    Vijana wakionyeshana ufundi

    Kocha Mkuu wa Azam Academy, Vivek Nagul akiwa na Msaidizi wake, Philipo Alando

    Vijana wakionyesha ufundi

    Mmoja wa |Maofisa wa benchi la Ufundi la Azam, Jemedari Said Kazumari

    MIraj Athumani wa Simba akikosa bao la wazi

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: AZAM AKADEMI WAICHAPA SIMBA B Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top