Kocha Kim Poulsen akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mechi leo |
KOCHA wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Kim
Poulsen amesema baada ya ushindi wa leo dhidi ya Gambia 'Nge' katika mechi ya kuwania
tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia 2014, sasa anaelekeza nguvu zake
katika mechi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika
dhidi ya Msumbji 'Mambas' wiki ijayo mjini Maputo.
Poulsen alisema amefarijika na ushindi wa leo akiiongoza
timu hiyo katika mechi ya tatu tangu aanze kazi, akirithi mikoba ya Mdenmark
mwenzake, Jan Borge Poulsen na anaamini sasa ana nafasi ya kucheza Kombe la
Dunia 2014 hivyo anajipanga zaidi ili kufanya vizuri.
Kim aliiambia BIN ZUBEIRY baada ya mechi ya leo,
ambayo mabao ya Shomari Kapombe wa Simba na Erasto Nyoni wa Azam kipindi cha
pili yaliifanya Stars itoke nyuma kwa 1-0 na kushinda 2-1 dhidi ya Gambia kwamba
kesho timu inaanza mazoezi kujiandaa na mechi na Msumbiji.
Poulsen amewataka vijana wake kutolewa sifa na badala yake
kuelekeza nguvu zao katika maandalizi ya mechi ijayo dhidi ya Msumbiji, kuwania tiketi ya kucheza Kombe la
Mataifa ya Afrika mwani Afrika Kusini.
Katika mchezo wa kwanza, Stars wakati bado inanolewa na Jan
Poulsen ililazimishwa sare ya 1-1 na Msumbiji nyumbani.
0 comments:
Post a Comment