• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    VILLARREAL YAJIKONGOJA TARATIBU

    Perez
    BAO la Hernan Perez dakika za majeruhi usiku wa jana, liliipa Villarreal ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Malaga, ushindi ambao unawaongezea matumaini ya kutoshuika daraja La Liga.
    Timu hiyo ambayo inajulikana kama 'The Yellow Submarine', ambayo inashika nafasi ya 17, imefikisha pointi saba kamili za kuwaweka salama kutoka eneo la hatari, baada ya kufikisha pointi 35 zikiwa zimebaki mechi sita.
    Villarreal ilimaliza katika nafasi ya nne msimu uliopita na kucheza Ligi ya Mabingwa, lakini imeshuka mno msimu huu na sasa ina kocha wa tatu kwa msimu huu mmoja pekee, Miguel Angel Lotina anayejaribu kuiepusha na balaa la kushuka daraja.
    Kiungo wao wa Paraguay, Perez alifunga bao dakika ya 94 kuiwezesha kuchukua pointi hizo, katika mchezo ambao kipa wa Malaga, Mcameroon Carlos Kameni alilimwa kadi nyekundu dakika ya 81.
    Kipa huyo wa Cameroon, alionyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumuangusha Perez kwenye eneo la hatari na Marcos Senna akafunga la kusawazisha kwa penalti.
    Mwanasoka wa kimataifa wa Hispania, Santi Cazorla, aliyekuwa chachu ya mafanikio ya Villarreal msimu uliopita, aliifungia bao la kuongoza Malaga dakika ya 65, lakini hakushangilia kukwepa kuwaudhi mashabiki wa timu yake ya zamani.
    Malaga, ambayo inamilikiwa na mtu wa Qatari, inabaki nafasi ya nne kwa pointi zake 50 na imeshindwa kuipiku Valencia yenye pointi 52 katika nafasi ya tatu. Valencia iliifunga Rayo Vallecano 4-1 juzi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VILLARREAL YAJIKONGOJA TARATIBU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top