• HABARI MPYA

    Thursday, April 05, 2012

    SIMBA WAHOFIA HUJUMA ALGERIA


    KATIKA kujihadhari na hujuma klabu ya soka ya Simba imeamua kuagiza mchele, maharage, maji na matunda kutoka Tanzania.
    Simba kwa sasa ipo nchini Algeria kujiandaa na mchezo wake wa marudiano wa Kombe la Shirikisho (CAF) dhidi ya Es Setif ya huko unaotarajiwa kupigwa wikiendi hii nchini humo.
    Mwenmyekiti wa Simba aliyeko huko amesema kuwa wameamua kuchukua tahadhari hiyo baada ya kukumbana na vitendo vya hujuma pindi waluipotua nchini humo.
    Alisema wapinzani hao wamepanga kuwahujumu kwa namna moja ama nyingine ili kuhakikisha wanashinda mechi hiyo na kusema kuwa wamejipanga kukabiliana na hila za waarabu hao na timu inaendelea vema na maandalizi ya mchezo huo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA WAHOFIA HUJUMA ALGERIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top