![]() |
| Del Piero kulia |
KLABU ya Juventus imerejea
kileleni mwa Serie A baada ya Alessandro Del Piero kufunga bao la dakika za
lala salama akicheza mechi ya 700 na kuiongoza klabu yake kushinda 2-1 nyumbani
dhidi ya usiku huu.
AC Milan iliifunga Chievo 1-0 jana
na kurudi kileleni kwa tofauti ya pointi mbili, lakini Juve sasa inaongoa tena
kwa tofauti ya pointi moja.
Awali, Lazio ilisawazisha kupitia
kwa Stefano Mauri baada ya Simone Pepe
kufunga la kuongoza.
Katika mechi nyingine, AS Roma iliwafunga
Udinese 3-1 wakati Napoli imefungwa 3-1 na Atalanta na Inter Milan imeifunga Siena
2-1, shukrani kwake Diego Milito aliyefunga mawili San Siro.
Cesena imetoka 1-1 na Genoa, Novara
imefungwa 2-0 na Parma, Lecce imeifunga 2-1 Catania
Inter sasa inalingana na Napoli katika
nafasi ya mwisho ya kuwania kucheza Europa League, huku kocha wake mpya, Andrea
Stramaccioni akishinda mechi ya pili katika mechi tatu tangu aanze kazi na Napoli
inashindwa kushinda kwa mara ya tano mfululizo kwenye ligi.



.png)
0 comments:
Post a Comment