• HABARI MPYA

    Wednesday, June 08, 2016

    MWENYEKITI ALGERIA AFUNGIWA MAISHA KWA KUPANGA MATOKEO

    MWENYEKITI wa klabu ya Abdelmadjid Yahi wa US Chaouia ya Algeria amefungiwa maisha kujihusisha na soka jana baada ya kusema kwenye Televisheni upangaji matokeo ulikithiri naye pia alishiriki.
    Mwezi uliopita, Abdelmadjid Yahi wa US Chaouia alilalamikia kushuka kwa timu yake hadi Daraja la Tatu akisema kulitokana na upangaji matokeo wa wazi.

    Abdelmadjid Yahi amefungiwa maisha baada ya kukiri hadharani aliwahi kushiriki kupanga matokeo ya mechi

    Kisha akasema yeye mwenyewe aliwahi kushiriki upangaji wa matokeo ya mechi siku za nyuma.
    Yahi, ambaye amekuwa Mwenyekiti wa US Chaouia kwa karibu miaka 25, alishughulikiwa na mamlaka za soka jana kwa kufungiwa maisha kujihusisha na soka pamoja na ktozwa faini ya dinar 200,000 (sawa na dola za Kimarekani 1,825 au Euro 1,600).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MWENYEKITI ALGERIA AFUNGIWA MAISHA KWA KUPANGA MATOKEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top