Ilianza hivi: Thomas Muller wa Ujerumani (kushoto) akipambana na Pepe wa Ureno kuwania mpira katika mchezo wa Kundi G Kombe la Dunia jioni ya leo mjini Fonte Nova, Salvador, Bahia, Brazil. Tazama mkono wa Pepe kwenye uso wa Muller. Ujerumani ilishinda 4-0
Muller akilalamika kuumia baada ya kukabiloiana na Pepe
Muller akajiangusha chini kiulaini akiwa ameshika uso wake
Pepe akakasirika na kumfuata Muller kumpa maneno
Pepe akaenda kumsukuma kwa kichwa Muller wakati ameketi chini
Muller akapiga kelele tena kulalamika kuumizwa tena kichwani
Muller akainuka na kuanza kuwekeana mkwara na Pepe
Kadi nyekundu: Pepe (wa pili kushoto) akionyeshwa kadi nyekundu huku Muller (kushoto kabisa) akizuiwa na mchezaji mwenzake, Toni Kroos asiende kugombana



.png)
0 comments:
Post a Comment