// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); IVORY COAST YAILAZA 2-1 JAPAN, ASANTE BONY NA GERVINHO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE IVORY COAST YAILAZA 2-1 JAPAN, ASANTE BONY NA GERVINHO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Sunday, June 15, 2014

    IVORY COAST YAILAZA 2-1 JAPAN, ASANTE BONY NA GERVINHO

    MABAO ya vichwa ya Wilfried Bony na Gervinho yaliyopishana kwa sekunde 98 yameipa mwanzo mzuri Ivory Coast katika Kombe la Dunia baada ya kuilaza Japan 2-1 katika mchezo wa Kundi C mjini Recife, Brazil.
    Tembo hao wa Ivory Coast walimuanzishia benchi Nahodha wake, Didier Drogba lakini ni kuingia kwake ndiko kulikuja sambamba na mabao hayo.
    Nyota wa Japan, Keisuke Honda aliifungia timu yake bao la kuongoza dakika ya 16 kabla ya Ivory Coast kusawazisha kupitiakwa Bony dakika ya 64 na Gervinho kufunga la pili dakika ya 65. Mapema katika mchezo uliotangulia jana wa kundi hilo Colombia iliiaza 3-1 Ugiriki.
    Kikosi cha Ivory Coast kilikuwa: Barry, Aurier, Bamba, Zokora, Boka/Djakpa dk75, Tiote, Yaya Toure, Die/Drogba dk62, Gervinho, Bony/Konan dk77 na Kalou.
    Japan: Kawashima, Uchida, Morishige, Yoshida, Nagatomo, Yamaguchi, Hasebe/Endo dk53, Okazaki, Honda, Kagawa/Kakitani dk86 na Osako/Okubo dk68.
    Mwanzo mzuri: Mshambuliaji wa Ivory Coast, Gervinho akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la ushindi alfajiri ya leo
    Pick that one out:  Keisuke Honda fires Japan ahead in the first half
    Mkali wao: Keisuke Honda akiifungia bao la kuongoza Japan
    On the charge: Yaya Toure looks to get forward and avoids the challenges of two players
    Mchezaji bora: Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure (katikati) akipambana na wachezaji wa Japan
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: IVORY COAST YAILAZA 2-1 JAPAN, ASANTE BONY NA GERVINHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top