• HABARI MPYA

    Thursday, April 05, 2012

    MOURINHO: NITARUDI INTER MILAN

    Mourinho
    KOCHA wa Real Madrid, Jose Mourinho amesema kwamba anapenda kurejea Inter Milan wakati Fulani katika maisha yake, lakini amesema hana mpango wa kuondoka Santiago Bernabeu kabla ya kumaliza mkataba wake wa sasa uliobakiza miaka miwili.

    Kocha huyo Mreno aliachana na Nerazzurri majira ya joto 2010 baada ya kuwapa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa, lakini bado ana hisia na vigogo hao wa Serie A.
    "Mimi ni shabiki mkubwa wa Inter. Klabu hiyo ni nyumbani kwangu na hakika nitarudi. Ligi? Hakuna cha kusema juu ya mustakabali wangu kwa sasa. Bado nina mkataba wa miaka miwili zaidi na Real na sijawahi kusema sitabaki Madrid," Mourinho alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MOURINHO: NITARUDI INTER MILAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top