TANZANIA imefanikiwa kuingia fainali michuano ya COSAFA Soka la Ufukweni baada ya ushindi wa 5-2 dhidi ya Angola leo ufukwe wa South Beach Arena Jijini Durban, Afrika Kusini.
Mchezaji wa Tanzania, Stephano Manyama amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo na sasa timu hiyo ya kocha Boniphace Pawasa itakutana na Msumbiji katika fainali Jumapili.
Msumbiji ambayo iliifunga Tanzania kwa penalti 4-3 baada ya sare ya 4-4 katika mchezo wa Kundi B jana, leo imewafunga wenyeji, Afrika Kusini 5-3 katika Nusu Fainali nyingine.
Reports: Jack Wilshere set for Arsenal return
-
Former Arsenal midfielder Jack Wilshere has held talks with the north
London side on one of its vacant academy coaching roles. Under 23 manager
Per Mertes...
YANGA ‘KUPAA’ JUMANNE KUIFUATA MWADUI FC
-
MARA baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc kwenye uwanja wa
Majaliwa, Lindi, siku ya jumapili, Kikosi cha Young Africans Sports Club,
kitareje...
0 comments:
Post a Comment