• HABARI MPYA

    Monday, November 01, 2021

    TANZANITE YAENDELEZA UBABE CECAFA


    TANZANIA imeendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya  CECAFA wanawake chini ya umri wa miaka 20 baada ya kuchapa Burundi 3-2 leo Uwanja wa FTC Njeru nchini Uganda
    Mabao ya Tanzanite leo yamefungwa na Mwamvua Haruna dakika ya 60 kwa penalti, Clara Luvanga dakika ya 80 na Emiliana Isaya dakika ya 83.
    Tanzanite iliyoshunda 1-0 dhidi ya Eritrea Jumamosi bao pekee la Clara Luvanga dakika ya 90 - itashuka tena dimbani Jumatano kumenyana na Ethiopia, kabla ya kuivaa Uganda Jumamosi na kukamilisha mechi zake kwa kucheza na Djibouti Novemba 9.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANITE YAENDELEZA UBABE CECAFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top